tecno

tecno

airtel

airtel

.

.

nido

nido

RADIO LISTEN NOW

24 Januari 2018


Pamoja na pesa ndefu wanayompa Sanchez, United bado namba 1 kwa utajiri duniani


Pamoja na kuanza kutoa kiasi cha £600,000 kila wiki kwa ajili ya nyota wao mpya Alexis Sanchez lakini hii haijawafanya Man United kuyumba kifedha na taarifa zinaonesha bado wako kilele cha klabu tajiri ulimwenguni.
Taarifa ya kifedha kutoka kwa shirika la Deloitte inaonesha kwamba Manchester United wanaongoza orodha ya vilabu tajiri ambapo kwa msimu 2016/2017 Manchester United wametengeneza kiasi cha £676.3m.
United wanakuwa wamewapiku Real Madrid kwa mara ya 10 na sasa Real Madrid wako nafasi ya pili kwani kwa msimu wa mwaka 2016/2017 matajiri hao wa Hispania waliweza kutengeneza pesa kiasi cha £674.6m.
Real Madrid wamekaa kwenye nafasi ya Barcelona na sasa Barca wameenda hadi nafasi ya tatu wakitengeneza kiasi cha £648.3m wakifuatiwa na mabingwa wa ligi ya Bundesliga waliotengeneza £587.8m.
Machester City vinara wa ligi kuu Uingereza wapo nafasi ya tano wakitengeneza mpunga wa £527.7m wakifuatiwa na Arsenal ambao 2016/2017 waliweka kibindoni jumla ya £487.6m.
Matajiri wa jiji la Paris(PSG) wako katika nafasi ya saba wakiwa wametengeneza pesa £486.2m, Chelsea wanafuatiwa na £428m, Liverpool £424.2m na Juventus nafasi ya 10 wanamalizia wakiwa wameingiza kiasi cha £405.7m.


Sanchez amponza Henry, mashabiki wataka sanamu lake livunjwe



Alexis Sanchez anazidi kuleta habari nyingi tangu ajiunge Manchester United, na sasa mshambuliaji huyo wa Chile amemuweka katika wakati mgumu mshambuliaji wa zamani wa Arsenal Thiery Henry.
Moja kati ya mambo ambayo Sanchez amesema wakati akijiunga na Manchester United ni ushauri alioupata kwa Thiery Herny ambapo Sanchez amedai kuzungumza na Henry kabla ya kuondoka.
Sanchez amesema Thiery Henry aliona ni sawa tu kwa yeye kuondoka Arsenal na Sanchez aliamua kufuata ushauri wa Thiery Henry na kuamua kuondoka Arsenal.
Mashabiki mtandaoni hii leo wengi wamekuwa wakimtupia Henry lugha chafu na wengine wakisema hawataweza kumtambua tena Thiery Henry kama legend wa timu ya Arsenal.
Mashabiki wengi wamedai kwamba Henry amekuwa akiwageuka mara nyingi na wengine wakikumbushia kwamba juzi tu aliwahi kumsifia Harry Kane wakati Tottenham ni wapinzani wao.
Sasa mashabiki wa Arsenal toka pande mbalimbali duniani wamekuwa wakiomba klabu ya Arsenal kuvunja sanamu la mchezaji huyo lililoko nje ya uwanja wa Emirates kwa kuwa Henry ni msaliti.

Valverde kumtumia Coutinho kuiangamiza Espanyol


Tangu Phillipe Coutinho ajiunge na klabua ya Barcelona akitokea Liverpool hajaonekana uwanjani kuitumikia klabu yake hiyo mpya lakini siku ya Alhamisi huenda akakata kiu ya mashabiki wa Barcelona.
Barcelona watakuwa na mchezo wa Copa Del Rey siku ya Alhamis ambapo watambana na Espanyol huku kocha wa Barcelona Ernesto Valverde akithibitisha kwamba huenda Coutinho akawepo katika mchezo huo.
Usajili wa Coutinho uliigharimu Barcelona kiasi cha £142 m lakini kutokana na majeraha aliyotoka nayo Liverpool walishindwa kumtumia kiungo huyo wa Brazil.
Kuanzia katikati ya wiki iliyopita Phillipe Coutinho amekuwa akifanya mazoezi na kikosi cha kwanza cha Barcelona na sasa kocha pamoja na madaktari wa timu hiyo wanaona yuko tayari kuanza kuitumikia Barcelona.
Katika mchezo uliopita Barcelona walifungwa bao moja kwa sifuri na Espanyol na kama wanahitaji nafasi ya kuendelea kuwepo katika michuano ya Copa Del Rey watahitaji kushinda mchezo wa Alhamisi.

Sahau kuhusu Sanchez, hawa wengine pia wamecheza chini ya Gurdiola na Mourinho


Leo kuna uwezekano mkubwa dili la Alexis Sanchez kwenda Manchester United kutoka Arsenal kukamilika, kama dili hii ikikamilika Sanchez atakuwa amecheza chini ya makocha wawili wakubwa EPL Pep Gurdiola na Jose Mourinho.
Kumbuka Alexis Sanchez kabla ya kwenda Arsenal, aliuzwa na Pep Gurdiola akitokea Barcelona lakini Sanchez hatakuwa mchezaji wa kwanza kucheza chini ya makocha hao wawili, wapo hawa nyota wengine.
 Xabi Alonso, kwa misimu mitatu Xabi Alonso aliitumikia Real Madrid chini ya Mourinho lakini kipindi chote hicho Pep alitamani kumnunua Alonso na alipofika Bayern Munich mwaka 2014 alimvuta Xabi Alonso.
Zlatan Ibrahimovich, hii ni mara ya pili kwa Ibrahimovich kuwa chini ya Mourinho, mara ya kwanza ilikuwa Inter Milan lakini Zlatan pia alicheza chini ya Pep Gurdiola mwaka 2009 akiwa Barcelona na uhusiano wao inatajwa kuwa ulivurugika hapo.
Cesc Fabregas, wakati Fabregas akitoka Arsenal iliaminika kwamba anakwenda kuwa Xavi mpya ndani ya Barcelona lakini msimu wake mmoja tu ndani ya Barcelona ulibuma na baadaye Pep Gurdiola alimuuza kwenda Chelsea akakutana na Jose Mourinho.
Kevin De Bruyne, kati ya wachezaji ambao watu wa Chelsea wanamlaumu sana Jose Mourinho ni Kelvin De Bruyne, Mourinho hakuelewa uwezo wa Mbelgiji huyu na haikuwa kazi kwake kumuacha aende Ujerumani lakini baadaye Man City waliamua kumrudisha na sasa yuko chini ya Pep Gurdiola.
Pedro, hadithi ya Pedro na ya Fabregas zinafanana fanana kwani Pep Gurdiola ndiye alitoa ruhusa kwa Pedro kuondoka Barcelona ambapo aliitumikia tangu akiwa na timh B nyota huyo alikwenda Chelsea kukutana na Jose Mourinho.
Samuel Etoo, kama ilivyo kwa Zlatan Ibrahimovich, huyu naye alicheza chini ya Mourinho mara mbili akiwa na Inter na pia Chelsea lakini pia nyota huyu wa Cameroon amewahi kucheza chini ya Pep Gurdiola alipouzwa kwenda Barcelona.
Maxwell, alipokuwa Inter alikuwa chaguo la kwanza la Jose Mourinho katika beki ya kushoto lakini baada ya msimu mmoja tu Maxwell alivutiwa na kwenda Barcelona kwenda kucheza chini ya Pep Gurdiola.
Claudio Pizzaro, wakati Jose Mourinho akikaribia kuondoka Chelsea mwaka 2007 huu ulikuwa usajili wake wa mwisho mwisho lakini baada ya kucheza sana soka mwishowe Pizzaro aliamua kujiunga na Bayern Munich chini ya Pep Gurdiola.

Alexis(United), Mkhi (Arsenal) yametimia


Baada ya siku takribani 10 za mvutano, majadiliano na fununu hatimaye jioni ya leo suala la Alexis Sanchez na Henrikh Mkhitaryan kwenda Manchester United limekamilika.
United wamemtangaza rasmi Sanchez kama mchezaji wao ambapo raia huyo wa Chile atakuwa akiweka £600,000 kila mwisho wa wiki kutoka kwa wababe hao wa jiji la Manchester.
Wakati Sanchez akitangazwa kuwa mchezaji mpya wa United, nyota huyo amesema anafuraha sana kuwa mchezaji wa kwanza kutoka Chile kuichezea klabu kubwa duniani.
Sanchez atakuwa anapokea mshahara wa £350,000 kila wiki huku akipewa kiasi cha £100,000 kila wiki itokanayo na haki za matangazo na pia atapewa bonus nyingine ya £140,000 kila wiki.
Wakati Sanchez akitangazwa na Manchester United hii leo, upande wa pili nako Henrikh Mkhitaryan ametangazwa na Arsenal kama mchezaji wao mpya.
Kwa mshahara wa Alexis sasa anakwenda kuwa mchezaji anayelipwa zaidi katika klabu ya Manchester United akiwa mbele ya Paul Pogba ambaye kwa sasa anapokea £220,000 kwa wiki.
Kwa upande wa Mikh aliyekwenda Arsenal amesema klabu hiyo ndiyo ilikuwa klabu ya ndoto zake na tangu akiwa mtoto mdogo alitamani siku moja kuvaa jezi ya Arsenal.


30 Oktoba 2017


Barcelona wametua nchini Ugiriki tayari kwa ajili ya mechi yao ya Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Olimpiakos.

Nahodha Lionel Messi amesema kikosi  chao kimejiandaa na wanachotaka ni ushindi.

Lakini amesisitiza, Olimpiakos si timu ya kubeza na kinachotakiwa ni kuhakikisha wanafanya juhudi







Manchester City inaonekana kuwa ndiyo timu inayotishia amani ya timu  nyingine Ligi Kuu England katakana na mwenendo wao.

City chini ya Pep Guardiola inaongoza msimamo lakini inaonyesha kuwa na rekodi nzuri zaidi.

Ndani ya mechi 10, imeshinda 9 na safe moja tu huku ikiwa na tofauti ya mabao ya kufunga na kufungwa 29, mambo linaloifanya timu yoyote inayotaka kuivuka lazima iwe kwa pointi.


Pia mwenendo wa kufunga mfululizo au katika njaa ya mabao kunaifanya City kuwa hatari zaidi Ligi Kuu England. Kwani inaonekana unapokutana na Manchester City hauwezi kujua nani atakudhuru.


Sergio Aguero amepachipa mabao saba kama ilivyo kwa Raheem Sterling na Gabriel Jesus na Leroy Sane kila mmoja amepiga mabao name, maana yake kwa washambulizi hao wane tayari ni jumla ya mabao 30.

Tambua wachezaji 5 Epl ambao bila pesa zaidi ya £100m huwanunui

1.Harry Kane. Thamani ya Kane inatajwa kukaribia thamani ya Neymar kwa sasa na Tot wanataka zaidi ya £170m kama unamtaka Kane, tayari Florentino Perez amekanusha kumhitaji Kane lakini ni wazi kwa umri wa Benzema na Cr7 lazima Perez atahitaji mtu hatari kuziba mapengo yao na ni Kane.
2.Phelippe Coutinho. Unafahamu kwamba Liverpool walikataa kiasi cha £118m kutoka kwa Barcelona? Ina maana Liverpool walitaka pesa kubwa zaidi ambapo Barca wanasema Liver walihitaji £200m na hii inamaanisha kwa sasa ni lazima uwe na kuanzia £118m ukimhitaji.
3.Kevin De Bruyne (KDB). Wakati Chelsea wakimuuza alionekana dogo wa kawaida tu lakini tangu City wamchukue kutoka Wolfburg anaonekana kati ya viungo bora kwa sasa duniani, kwa uwezo wake na thamani ya Man City baasi bila shaka ukiwa na kuanzia £110m City wanaweza kufikiria kukupa.
4.Dele Alli. Real Madrid wanamtala Ai na Kane kwa pamoja na sio rahisi hata kidogo kwani zaidi ya £240m zinaweza zikawatoka kuwanasa wote wawili, umri mdogo wa Ali, kiwango kikubwa akiwa ameweka kambani mabao 31 toka aanze Epl itakupasa uwe na £100m kumpata.
5.Eden Hazard. Jana tu ametoka kuwaumiza Fc Bournamouth bao pekee na kiwango chake kinaonekana kuzidi kuimarika baada ya majeraha msimu uliopita, Real wanamtaka na Hazard na Chelsea wako tayari kufikiria ada ya £100m.

Jose Mourinho akerwa na aina hii ya mashabiki wa Manchester United


Kocha wa Manchester United Jose Mourinho amewatupia lawama mashabiki wa klabu ya Manchester United kwa kitendo cha kutokumuunga mkono mshambuliaji wao Romelo Lukaku.
Jose Mourinho anasema ameshangazwa sana na mapokezi ya Lukaku katika mchezo dhidi ya Tottenham na kusisitiza kwamba sio jambo la kiungwana kufanya hicho wanachofanya mashabiki wa United kwa sasa.
Mourinho anasema Romelu Lukaku anawapa Manchester United kila kitu alichonacho na anapambana kwa ajili ya timu hivyo haoni sababu ya mashabiki hao kumfanyia roho mbaya mchezaji huyo.
Mourinho amewataka mashabiki wa United kukumbuka mabao aliyowafungia klabu hiyo na kusema kwamba kwa anavyojitolea Mbelgiji huyo hakuna tofauti akifunga mabao na asipofunga.
Mourinho amesema anahisi mashabiki ambao wanamponda Romelu Lukaku kwa sasa watakuwa sio mashabiki wa Manchester United na labda watakuwa na klabu nyingine, Lukaku ana mechi 3 sasa za Epl hajafunga bao lakini ana mabao 7 katika mechi 10 alizoichezea United tangu ajiunge nao.

15 Oktoba 2017

George Weah akaribia uraisi wa Liberia


Matokeo ya uchaguzi nchini Liberia yameanza kutoka huku mshambuliaji wa zamani wa klabu za PSG,Monaco na Chelsea George Weah akionesha kuongoza kwa kura nyingi.
Bado kura nyingi hazijahesabiwa lakini hadi sasa George Weah anaongoza katika majimbo 11 kati ya 15 ambayo tayari kura zao zimekamilika humu idadi kubwa ya majimbo kura zikiwa hazijahesabiwa.
Habari njema na ya matumaini kwa George Weah ni kwamba mpinzani wake mkubwa ambaye pia ni makamu wa raisi wa nchini hiyo Joseph Boakai anaongoza katika jimbo moja tu.
Ili mshindi apatikane inatakiwa apate kura zaidi ya 50% ya kura zote na George Weah inaoenakana wazi anaweza kuwa raisi wa kwanza kuwahi kushinda Ballon D’Or.
Wiki hii kumekuwa na tetesi nyingi kuhusu ushindi wa Weah ambapo hata kocha Arsene Wenger alizipata fununu kuwa Weah ameshashinda uchaguzi na akaamua kumpongeza jambo ambalo halikuwa kweli.

Getafe kumpa Zinedine Zidane rekodi mpya Real Madrid


Hakuna aliyedhani kwamba Zinedine Zidane anaweza kuwa kati ya makocha wakubwa duniani, wengi waliamini Zidane asingeiweza Real Madrid na wakiamini baada ya muda anaweza kutimuliwa.
Lakini tangu January 4 2016 wakati Perez akimkabidhi timu Zidane amekuwa akiwaonesha watu kwamba haikuwa bahati mbaya kupewa Real Madrid na ilikuwa sahihi kwake kupewa timu.
Kwa sasa Zinedine Zidane siyo yule ambaye siku 600 zilizopita wachambuzi wengi duniani walikuwa hawaamini kwamba atafanya vizuri kwani sasa anatajwa kama mmoja wa makocha bora duniani.
Wikiendi hii Zinedine Zidane anaweka rekodi katika klabu ya Real Madrid ambapo mchezo wake wa leo dhidi ya Getafe utamfanya Mfaransa huyo kufikisha idadi ya mechi 100 tangu apewe ukocha mkuu.
Takwimu zinaonesha Zinedine Zidane ni kocha aiyefanya makubwa zaidi Real Madrid akiweka rekodi kuwa kocha wa kwanza kutetea Champions League na katika michezo yake 100 ameipa Madrid makombe 7.
Zinedine Zidane ndiye kocha aliyekata kiu ya miaka mitano ya Real Madrid kuchukua ubingwa wa La Liga huku akiwapa pia Europeans Cup mara mbili, klabu bingwa dunia na Spanish Super Cup.

Jose Mourinho kuchezesha mlinzi mmoja na washambuliaji 9 dhidi ya Liverpool


Liverpool wanaikaribisha Manchester aunited siku ya Jumamosi katika uwanja wa Anfield,mchezo huu mara zote unakuwa wa upinzani mkubwa haijalishi timu zitakuwa katika viwango gani.
Kwa kipindi hiki cha sasa waandishi wengi wa habari barani Ulaya wanajaribu kutafuta habari kupitia Jose Mourinho ambaye mara nyingi hakosi cha kusema wakati wa kuelekea katika mipambano mikubwa.
Hii leo Mourinho ametoa mpya baada ya kuulizwa ni mfumo gani anaenda kuutumia katuka mchezo huu wa Jumamosi na ndipo Mourinho alipotoa jibu ambalo limekuwa kichwa cha habari kila sehemu.
Jose Mourinho aliwaambia waandishi wa habari kwamba wasiwe na shaka kwani safari hii anakwenda Anfield na mfumo mpya ambapo ataweka mlinzi mmoja huku mbele akiweka washambuliaji tisa.
Wengi wamelichukulia jibu la Mourinho kama utani lakini kwa kumbukumbu jibu hili linaonekana kama kijembe cha wale waliomponda msimu uliopita alipokwenda Anfield kwamba alienda kupaki basi.
Mourinho pia amesisitiza kwamba kusema kwamba hii ndio mechi yao ya kwanza na timu kubwa/ngumu haiwaathiri wao lakini sio sawa kwa wapinzani ambao wameshacheza nao na ni kuwashushia heshima.
Wakati huo huo Mourinho amesema Michael Carrick naye hatakuwepo katika mchezo wa kesho dhidi ya Liverpool kutokana na ugonhwa lakini mshambuliaji wao Romelu Lukaku yuko fiti kuikabili Liverpool.

Mambo matano niliyoyaona EPL Jumamosi hii


1.United wanazuilika kabisa, ilikuwa suluhu 3 ambayo haikuwa na mabao kati ya Liverpool na Manchester United, lakini mchezo wa leo Anfield umeonesha United wanaweza kuzuilika kabisa huku walinzi wa Liverpool wakimpoteza nyota wao Romelu Lukaku,ni wazi United kama sio De Gea wangekufa.
Katika suluhu hiyo mlinzi wa kulia wa Manchester United Antonio Valencia aliweka rekodi kuwa mchezaji wa kwanza ambaye sio mzaliwa wa bara la Ulaya kuichezea United michezo 300.
2.Chelsea kama popo, Goli la kuongoza la Crystal Palace liliwafanya Palace kukomesha njaa yao ya ufungaji ambayo imedumu kwa muda wa masaa 12 na hilo lilikuwa bao lao la kwanza kupata katika mashuti 86 waliyopiga msimu huu.
Chelsea msimu huu imekuwa  haieleweki kwani kuna wakati wanaonekana wamechoka sana lakini kuna wakati wanaonekana kujaribu kurudi, kipigo cha leo kimewarudisha nyuma kwani wangeshinda wangepunguza pengo la alama na timu zilizoko juu yao.
3.Pep anataka kombe tu sio hadithi, Etihad panaonekana sasa sio mahalinpakwenda kabisa, wapinzani, timu mbili kabla ya Stoke zilizofika Etihad zilikufa bao 5 huku leo Stoke City akila 7 kwa 2 ambazo kwa mahesabu mengine ni sawa na 5 bila, usajili aliofanya na matokeo anayopata vinaonesha wazi anataka ndoo.
4.Wenger arudi kwenye sack race, Arsenal Wenger ameanzishiwa tena mabango ya Wenger Out ambayo yalishaanza kupotea, kipigo cha bao 2 kutoka kwa Watford kimeamsha hisia kali kwa mashabiki wa klabu hiyo na wameshaanza kutuma  ujumbe wa Wenger out mitandaoni na sasa anarejea katika mbio za kufukuzwa.
5.Wembley sio parahisi kwa Tottenham, mashabiki wa Tottenham hawapapendi Wembley na wengi wanaamini wana mkosi na uwanja huo, leo wamepata ushindi wao wa kwanza katika uwanja huo.
Lakini kwa Tottenham ya sasa ilikuwa wazi kwamba kucheza na timu ya chini kama Afc Bournemouth kulitarajiwa mabao mengi lakini wamepata ushindi mwembamba sana wa bao mja dhidi ya Bournemouth.

“Della Madonnina” moja kati ya derby kubwa ulimwenguni kupigwa hii leo


Nchini Italia leo hatumwi mtoto dukani, leo ni siku kubwa kwa Waitalia wemgi kuuona mpambano wenye historia kubwa sana ambapo derby ya Della Madonina ndio habari ya Italia kwa hii leo.
Katika ligi kuu nchini Italia Serie A Inter Millan wanaonekana wababe zaidi wa Ac Millan, michezo 166 waliyokutana vigogo hawa Inter waliibuka kidedea mara 61 huku Ac wakishinda mara 51 na suluhu 54.
Lakini kiujumla timu hizi mbili katika michuano yote zimekutana mara 218 tangu mwaka 1929 na katika mechi hizo Inter Millan wameshinda mara 77 ikiwa ni mara mbili tu zaidi ya Ac Millan walioshinda michezo 75 hali inayoonesha ulinzani kati ya miamba hii.
Katika derby hii kipigo kikubwa kabisa kutokea ilikuwa mwaka 1910 ambapo Inter Millan waliinyuka Ac Millan mabao 5 kwa nunge, japokuwa Ac Millan nao walilipa kipigo hicho mwaka 1960.
Safari hii timu hizi zinakutana katika mazingira tofauti kabisa na mwanzo ambapo safari hii Derby Della Madonnina inawakutanisha Ac Millan na Inter huku zote zinamilikiwa na makampuni ya uwekezaji toka China.
Andriy Shevchenko ndiyo mchezaji anayeongoza kwa kupiga mabao mengi katika Derby hii akifunga mara 14 huku Giussepe Meaza akifuatia na mabao 13 yeye alitafunga mabak haya akizichezea klabu zote mbili.
Juventus na Ac Millan wanafanana sana mambo mengi kwani wote wana makombe 18 ya Serie A, wote wana makombe 15 ya bara la Ulaya lakini pia wote wawili wana makombe 12 ya Copa Italia.
Na kama hufahamu tu ni kwamba katika miaka mitano iliyopita klabu ya Ac Millan imefukuza makocha sita ambapo mapacha wao wa Inter Millan wao wamefukuza makocha watano.
Ac Millan watajaribu kupata ushindi ili kuikaribia Inter walioko nafasi ya pili Serie A huku hawajapoteza mchezo hata mmoja na Ac Millan wako nafasi ya 7 wakiwa na alama 12 huku wakiwa wamepoteza michezo mitatu.

13 Oktoba 2017

Lukaku anaweza kuweka rekodi hii? Koeman atatimuliwa? Haya ni baadhi ya maswali ya kujiuliza kuelekea weekend ya Epl


Michezo ya kufuzu kwa fainali za kombe la dunia kwa wiki hii imemalizika na sasa tunakwenda katika ligi za vilabu, na kati ya wiki tamu katika soka ni wiki hii kwani mitanange mingi itakuwa moto moto.
Klopp atafanyaje dhidi ya United? Liverpool watakipiga dhidi ya Manchester United,mchezo huu unaweza kuwa na presha kubwa kwa Jurgen Klopp kutokana na matokeo anayoyapata siku za karibuni huku mshambuliaji muhimu Sadio Mane akiwa majeruhi.
Eneo la ulinzi haliko vizuri na Klopp analijua hilo,tusubiri kuona kama amelifanyia kazi eneo hilo au ataendelea kudoda mbele ya United wanaoonekana kuwa na washambuliaji viwembe.
Romelu Lukaku kuwa mchezaji wa kwanza kuweka rekodi hii? Tayari amefunga katika michezo 7 mfululizo ya Epl na huu ni mchezo wake wa 8 na kama akifunga atakuwa mchezaji wa kwanza kufunga katika michezo yake 8 ya mwanzo na timu mpya Epl.
United watachezaje bila Pogba na Fellaini? Baada ya Paul Pogba kupata majeraha kocha wa Manchester United alianza kumuamini Marouane Fellaini na sasa Fellaini naye ameumia huku hofu ya majeraha ikianza kuwatesa, Ander Herrera huenda akapewa nafasi na watu wanasubiri kuona nini atafanya.
Tottenham watapata alama 3 kwa mara ya kwanza Wembley? Wembley uwanja wa nyumbani wa Tottenham utawakaribisha Bournemouth, lakini Wembely pamekuwa pagumu mno kwa Tottenham na hawajawahi kupata alama 3 msimu huu na wiki hii wanatari labda wanaweza kuzipata.
Etihad kuendelea kuwa mahala pa kukatili wapinzani? Stoke City anakanyaga Etihad huku wageni wawili waliopita hapa walikula bao tano tano kila mmoja, Stoke wanaenda wakiwa wanayumba yumba nao wanaweza kupata walichopata waliotangulia.
Arsenal wataendeleza vipigo? Michezo minne iliyopita ya Arsenal wanaonekana kuanza kukaa vizuri, Jumamosi hii wataifuata Watford huku Alexis Sanchez akitoka kwenye majonzi ya kulikosa kombe la dunia lakini pia tunasubiri kuona kama Wenger atampa nafasi Wilshaire anayeonekana kutoswa Arsenal.
Brighton watamfukuzisha kazi Ronald Koeman? Ndio/Hapana hili linaweza kutokea, Everton wanaweza kuwa wamechoshwa na matokeo wanayopata ukizingatia kwamba walitumia kiasi kikubwa cha pesa kufanya usajili lakini pia wanaweza kuendelea kumpa muda Koeman aijenge timu.

Raisi wa PSG aingia katika kesi kubwa ya kutoa rushwa


Taifa la Qatar bado linaandamwa na kesi ya rushwa, Qatar wabadaiwa kwamba walitoa rushwa ili wapewe nafasi ya kuandaa michuano ya soka ya kombe la dunia mwaka 2022 suala ambalo liliwaandama sana.
Nasser Al Khelaifi tajiri wa Qatar ambaye ndiye raisi wa klabu ya PSG naye ameingia katika kesi ya rushwa ambapo inadaiwa alitoa kiasi kikubwa cha pesa kwa moja wa maafisa wa FIFA ili kupewa haki za matangazo.
Al Khelaifi ambaye majuzi tu aliishangaza dunia kwa kufanya usajili uliovunja rekodi ya dunia kumnunua Neymar anadaiwa kwamba alihitaji kumiliki haki za kurusha matangazo ya michezo ya kombe la dunia mwaka 2026 na 2030.
Jerome Vackle aliyekuwa secretary wa zamani wa chama cha soka duniani FIFA anadaiwa alipewa kiasi cha pesa kwa ajili ya kulisaidia shirika la Bein Sports kupata haki za matangazo hayo ya kombe la dunia.
Kuhusishwa kwa Al Khelaifi na kesi hii kunazidi kuiweka Qatar karibu skendo ya rushwa katika fainali za kombe la dunia 2022 ambapo kesi ya Vackle naye ambaye alitimuliwa na FIFA kutokana na kesi za rushwa anazidi kuchafuka.
Maofisa wa masuala ya rushwa kutoka Uswisi wamesema El Khelaifi ambaye ni bosi wa shirika la Bein Sports alilitumia shirika lake kama njia ya kupata tenda hiyo ya matangazo ya kombe la dunia na tayari maofisa hao wameanza uchunguzi dhidi ya Al Khelaifi.
Bado hadi sasa raisi huyo wa PSG hajazungumza lolote juu ya madai dhidi yake japo hii inaweza kuwa kesi kubwa itakayomchafua yeye pamoja na Qatar kuelekea fainali za kombe la dunia mwaka 2022.

Romelu Lukaku ana rekodi mbovu dhidi ya Liverpool na Jose Mourinho ni kibonde wa Klopp, lakini je Liva hii itaweza izuia United ya sasa?


Tangu mwaka 2014 pale Liverpool walipoipiga Manchester United bao 3 kwa 0 klabu hiyo haijawahi kupata ushindi tena dhidi ya Manchester United kwenye mechi zilizofuata za Premier League.
Jumamosi hii wanakutana tena Anfield na safari hii United wanakuja Anfield wakiwa wanajiamini kwanj katika michezo mitano iliyopita waliyocheza hapo United wameshinda mara 3 wakipata suluhu 1 na kupoteza mara 1.
Kama Liverpool wakipoteza mchezo huu itakuwa habari mbaya kwa Klopp kwani 2014 Brenden Rodgers alifukuzwa baada ya kupata alama 12 katika mechi 8 sawa na ambazo Klopp atazipata kama akipoteza mchezo huu.
Lakini Jurgen Klopp anawapa matumaini Liverpool kutokana na rekodi nzuri mbele ya Mourinho kwani katika michezo 7 Mou amemfunga Klopp mara moja tu huku wakisuluhu mara 3 na Klopp akishinda 3.
Manchester United wanaoonekana kutaka kuendeleza wimbi la ushindi wanaweza kuweka rekodi mpya ya kufikisha alama 22 katika michezo 8 ya Epl kama wakiibuka kidedea dhidi ya Liverpool.
United watakuwa na mshambuliaji wao Romelu Lukaku ambaye siku za usoni anaonekana kujenga urafiki na nyavu na kama akifunga atakuwa mchezaji wa kwanza Epl kufunga mfululizo katika mechi 8 za mwanzo.
Lakini pamoja na ukali wake wote wa kufunga Romelu Lukaku huwa anapata wakati mgumu sana mbele ya Liverpool ambapo katika michezo 7 aliyocheza dhidi ya Liverpool amefanikiwa kufunga bao moja tu.
Manchester United watawakosa Paul Pogba na Maroane Fellaini huku ngome yao ya ulinzi ikiwapa jeuri kubwa ambapo kwa mwaka huu tu 2017 wana clean sheets 17 idadi ambayo hakuna klabu waliyoifikia.
Ni mchezo ambao sio mrahisi kwa pande zote kwani Liverpool pamoja na kumkosa Sadio Mane lakini Mo Salah yupo na Coutinho yupo huku United Ander Herrera anaweza kuanza lakini mashaka makubwa yapo katika eneo la ulinzi la Liverpool linaloonekana kupwaya mno, dakika 90 zitaamua.

Kuelekea mpambano wa Liverpool vs Manchester United, Juan Mata afanya jambo kubwa kwa watoto maskini


Manchester United wanakwenda Anfield kuikabili Liverpool Jumamosi hii, mchezo ni mgumu na unataraji kuvuta hisia za watazamaji wengi ulimwenguni kutokana na upinzani na historia baina ya timu hizi mbili.
Wakati wachezaji na mashabiki wakijiandaa na mchezo huu kwa wiki hii, hali ni tofauti kwa kiungo mnyumbulifu wa Manchester United Juan Mata ambaye wiki hii alikuwa na ugeni mkubwa uwanjani Old Traford.
Juan Mata alisafirisha kundi la watoto maskini ambao wanacheza soka kutoka India akawaleta Uingereza ili kuja kuona Old Traford na kupiga picha katika maeneo mbali mbali ya uwanja huo na kujifunza kuhusu soka.
Ziara ya watoto hawa inakuja baada ya miezi michache iliyopita kiungo huyu alipotembelea mji wa Mumbai na kuona mazingira magumu wanayoishi watoto hawa na ndipo aliamua kuwaleta OT kama njia ya kuwahamasisha kufikia malengo yao.
Juan Mata ameamua kuwasaidia watoto hawa kwa kuwahamasisha kuhusu kucheza soka lakini pia kuwapa elimu ya maisha na darasani mpango ambao tayari baadhi ya nyota wakubwa duniani wameanza kumuunga mkono.
Juan Mata aliwaalika Ander Herrera na nyota wa zamani wa United anayekipiga Everton Morgan Schnerdelin kujumuika pamoja na watoto hao pamoja na kupiga nao picha kabla ya kuwapeleka katikati ya uwanja wa Old Traford.
Katika kuendeleza suala hilo Juan Mata amewaomba wacheza soka wenzake kuchangia hata 1% ya kipato chao ili kuwasaidia watoto wasio na uwezo huku akisema anaaamini wachezaji wenzake wa Manchester United watamuunga mkono.
Mlinzi wa Juventus Giorgio Chiellini amemtumia Juan Mata salamu za kumunga mkono kwa kile anachokifanya huku pia Matt Hummels wa Bayern Munich, Serge Gnabry wa Hoffnheim  nao wakiunga mkono kampeni hii ya Juan Matta.

Achana na Liverpool vs United, hii ni michezo 4 ambayo hupaswi kukosa wikiendi hii



Sahau kuhusu Liverpool watakapoikaribisha Manchester United pale Anfield, lakini hii inaweza kuwa wikiendi tamu zaidi katika ligi za barani Ulaya tangu kuanza kwa msimu huu wa 2017/2018.
1.Lyon vs Monaco, wenyeji Lyon wako katika nafasi ya 8 ya ligi na watawakaribisha Monaco walioko nafasi ya 2 katika Serie A, Lyon wamepoteza mchezo mmoja msimu huu sawa na Monaco lakini wamesuluhu mara 3 zaidi ya wapinzani wao.
2.Borussia Dortmund vs Rb Leizp, BvB wamekusanya alama 19 katika michezo 7 ya Bundesliga ikiwa na maana kwamba wameacha alama mbili tu, tangu msimu uanze mwaka huu hawajawahi kudondosha alama 3.
Lakini Rb Leizp wakiongozwa na mshambuliaji anayekuja kwa kasi duniani Timo Werner watajaribu kutafuta ushindi wa 3 mfululizo katika Bundesliga huku wakijiamini kutokana na matokeo mazuri msimu uliopita.
3.Roma vs Napoli, katika michezo 36 waliyocheza klabu ya As Roma wanaonekana wababe wa Napoli ambapo wameshinda michezo 18 kati ya 36 huku Napoli wakishinda michezo 9 na wametoka suluhu mara 9 na wikiendi hii Roma watakuwa Stadio Olimpico kujaribu kuendeleza utemi.
4.Atletico Madrid Vs Barcelona, Diego Simeone ana rekodi mbovu sana dhidi Barcelona ambapo katika michezo 21 amepata ushindi mara mbili tu na safari hii anawakaribisha Barcelona ambao msimu huu wanaonekana hawashikiki.
Barcelona wamekusanya alama zote 21 katika michezo yao 7 katika La Liga huku Atletico walioko nafasi ya 4 nao hawajapoteza mchezo hata mmoja lakini wamesuluhu mara 3 na kupata jumla ya alama 14.

Msiompenda Cr7, rekodi zinaonesha huu ni mwezi mbaya kwenu


Msimu wa La Liga umeanza vyema kwa Lioneil Messi na Barcelona huku upande wa pili Cristiano Ronaldo akianza kwa kusua sua katika michuano hii ya La Liga jambo linalowaumiza mashabiki wake.
Lakini rekodi hazidanganyi na rekodi zinaonesha kwamba mwezi huu wa 10 huwa ndio mwezi ambao Mreno huyu huutumia kufanya makubwa na ndio mwezi ambao wapinzani wa Ronaldo huteseka.
Mwaka 2010 mwezi kama huu Cr7 alifunga hatrick nne na 2011 mwezi wa 10 Cristiano Ronaldo aliweka rekodi baada ya kufunga mabao 10 katika michezo 4 ya ligi kuu nchini Hispania La Liga.
Msimu wa mwaka 2014/2015 katika mechi mbili za La Liga Cr7 aliweka kambani bao 6 na kudhihirisha kwamba yeye ndio mfalme wa mwezi October.
Malaga wamekuwa wahanga wakubwa wa Cristiano Ronaldo katika mwezi wa 10 ambapo amewafunga mara 6, wakifuatiwa na Levante aliowaua mara 4 huku Barcelona,Sevilla, Alaves akiwafunga mara tatu tatu.
Mwezi huu Eibar, Girona na Getafe watakutana na Cr7 huku Tottenham Hotspur nao watakutana na Cristiano Ronaldo katika mwezi ambao anaogopesha na kwa kuanzia wataanza Gdtafe siku ya Jumamosi.

Hiki ndicho kilichopelekea Pochettino kusema “Gurdiola hana nidhamu na anapenda kuwadharau wenzake” 



Kocha wa klabu ya Tottenham Hotspur Maurcio Pochettino ameonekana kuchukizwa na maneno yaliyotolewa na Pep Gurdiola na kusema hadharani kwamba anahisi kukosewa heshima na kocha huyo.
Haya yamekuja baada ya Pe Gurdiola kuipa Tottenham Hotspur jina jipya la “Timu ya Harry Kane” kitendo ambacho Pochettino amekitafsiri kama muendelezo wa Pep Gurdiola kudharau watu wengine.
Pochettino amesema anamjua vyema Pep Gurdiola tangu kabla hajajiunga na Barcelona na anaamini katika uwezo wa kocha huyo lakini anafahama Pep hana nidhamu na amekuwa hivyo kwa watu wengi.
Pochettino amesema anashangazwa sana na kitendo cha kocha huyo kuwaita “Timu ya Kane” wakati yeye mafanikio yake makubwa alipokuwa Barcelona yaliletwa na Lioneil Messi lakini hakuna aliyewaita “Timu ya Lioneil”
Pochettino amesema mafanikio ya timu sio mtu mmoja na maneno kama aliyosema Gurdiola yanawakera watu wengi na wengi wanajisikia vibaya na kuchukulia maneno hayo kama ukosefu wa nidhamu.
Kocha huyo wa Tottenham amesema wakati wa mapumziko katikati ya wiki alikuwa kimya akiamini Pep atampigia simu kuomba msamaha lakini kocha huyo hakufanya hivyo lakini akisema hilo halijawaathiri wachezaji wameishia kucheka.
Harry Kane amekuwa na misimu mizuri sana siku za usoni huku msimu huu akiwa ameweka kambani magoli 15 katika michezo 10 na pia akifunga mabao 11 kati ya 16 ya Tottenham msimu huu hali inayowafanya wengi kuamini anaibeba Tottenham.