WBA-UKIMTAKA MZAWA WA BUJUMBURA SAIDO BERAHINO WEKA PAUNI MILIONI 30 MEZANI!
Berahino, Mzaliwa wa Bujumbura, Burundi mwenye Miaka 21 ambae
alikulia Uingereza, sasa anaichezea Timu ya Taifa ya England baada ya
kuanza kuvichezea Vikosi vya Vijana vya Nchi hiyo kuanzia vile vya U-16
na kupanda hadi kuichezea Timu ya Kwanza.
Hivi sasa Berahino na WBA wana mvutano kuhusu Mkataba mpya ambao
Straika huyo amegoma kusaini huku akiwa amebakiwa na Miaka Miwili katika
Mkataba wake wa sasa.
Hadi sasa, Berahino anaviziwa na Klabu za Newcastle, Tottenham, Arsenal, Man City na Chelsea.
Klabu nyingine ambayo ina nia ya kumsaini Berahino ni Liverpool
lakini hili lina utata na litakuwa gumu kwa vile Wakala wa Mchezaji huyo
ni Aidy Ward ambae pia ni Wakala wa Raheem Sterling wa Liverpool na
tayari Wady ana bifu kubwa sana na Liverpool kiasi cha kutangaziana vita
kuhusu sakata la Sterling kugomea Mkataba mpya na kushikilia kuhama.
Msimu wa 2014/15, Berahino ameifungia WBA Mabao 20.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni