tecno

tecno

airtel

airtel

.

.

nido

nido

RADIO LISTEN NOW

25 Juni 2015

MRITHI WA DE GEA NJIANI KUTUA OLD TRAFFORD!!

OLD-TRAFFORDZipo ripoti nzito toka England zinazodai Meneja wa Manchester United Louis van Gaal na Kipa wa Tottenham Hugo 9f2cea0a79ad90df14f74329847baabcLloris wamefikia muafaka na Kipa huyo wa Kimataifa wa France ambae ameshakubaliana kuhusu maslahi yake binafsi huko Old Trafford.
Huku kukiwa na mipango ya chini chini ya Kipa Nambari Wani David de Gea kurudi kwao Spain kuidakia Real Madrid, kumchukua Hugo Lloris kunaelekea kuziba pengo hilo.
Kwa mujibu wa chanzo cha habari hizi, Gazeti linaloheshimika huko France L'Equipe, kilichobaki sasa ni mazungumzo ya kukubaliana Ada ya Uhamisho na Mwenyekiti wa Tottenham Daniel Levy.
L'Equipe imedai Levy amemhakikishia Lloris kuwa Klabu yeyote itakayotoa Ofa ya Pauni Milioni 18 kwenda juu basi atamruhusu kuhama White Hart Lane.
Lloris, mwenye Miaka 28, alijiunga na Tottenham Mwaka 2012 akitokea Lyon ya France kwa Dau la Pauni Milioni 11.4.
Hata hivyo, Levy anasifika mno kwa ugumu wa kutoa Wachezaji wake Nyota na kama akiwaruhusu basi Dau lao huwa sio masihara.
 

UHAMISHO-OSPINA, NANI KUELEKEA UTURUKI? OBI NAE NJIANI UAE?

Work-pics1971Hiki ni kipindi cha kurushwa habari za kila aina za Uhamisho wa Wachezaji Mastaa na huko England zipo ripoti zinazowahusu Kipa wa Arsenal, David Ospina, na Winga wa Manchester United, Nani, wote kutua Uturuki huku Kiungo wa Mabingwa Chelsea, Mnigeria John Mikel Obi, akitajwa kuelekea UAE, Falme za Nchi za Kiarabu.Nani-celeb-Chelsea-v-Manchester-United-Capita 2853864
Ospina na Nani kutua Fenerbahce?
Kipa wa Arsenal, David Ospina, anedakia Timu ya Taifa ya Colombia, ametoboa kuwa yuko kwenye mazungumzo na Klabu ya Uturuki  Fenerbahce.
Kuondoka huku kwa Ospina ni kumpisha Kipa wa Chelsea Petr Cech kuhamia Arsenal wakati kukiwa na ripoti kuwa Uhamisho huu uko njiani kukamilika.
Ospina alihamia Arsenal Mwezi Januari akitokea Klabu ya France Nice na kumvua Jezi Nambari Wani Wojciech Szczesny kwa kucheza Mechi 18 za Ligi Kuu England.
Lakini ujio wa Cech na Szczesny kung'ang'ania kubaki Arsenal kumemfanya Ospina asake njia ya kwenda.
Wakati huo huo, Winga kutoka Ureno wa Manchester United, Nani, mwenye Miaka 28, yupo njiani kujiunga na Fenerbahce ikiwa mazungumzo kati ya Klabu hizo mbili yatakamilika.
Nani amepewa Ofa ya Mkataba wa Miaka Minne na Mshahara wa Pauni 55,000 baada ya Kodi na Fenerbahce ambayo iko tayari kuilipa Man UNited Pauni Milioni 7 kwa Uhamisho wake.
David-Ospina
John Obi Mikel
Baada kutupwa Benchi kufuatia uamuzi wa Meneja Jose Mourinho kuwapendelea Viungo Nemanja Matic na Cesc Fabregas, Kiungo wa Nigeria John Mikel Obi ameamua kutimkia UAE, Falme za Nchi za Kiarabu, na kujiunga na Al Ain.
Obi alicheza chini ya nusu ya Mechi za Ligi wakati Chelsea wakitwaa Ubingwa wa Ligi Kuu England msimu uliopita na hilo limemkera sana Mnigeria huyo.
 

EVERTON WAMPATA DEULOFEU WA BARCA, LIVERPOOL WANASA WA 6, MAN UNITED WAONGEA NA REAL KUHUSU RAMOS!

Nathaniel-Clyne-009Mbio za kunasa Wachezaji wapya katika KIpindi hiki cha Dirisha la Ulamisho na Leo Everton imethibitisha kumnasa Winga Chipukizi wa Barcelona huku Liverpool wakinyemelea kumsaini Mchezaji mwingine mpya wakati Manchester United wakitoa Ofa ya kumnunua kigogo wa Real Madrid.
Fowadi wa Barcelona Gerard Deulofeu 
Everton wamemsaini Fowadi wa Barcelona Gerard Deulofeu kwa Dau la Pauni Milioni 4.3.
Deulofeu, mwenye Miaka 21 na ambae ameichezea Spain mara 1, alikuwa na Everton kwa Mkopo Msimu wa 2013/14 na kisha kurejea Barcelona ambapo Msimu uliopita alipelekwa tena nje kwa Mkopo safari hii huko Sevilla.
Mchezaji huyo ataanza kuwa Mchezaji rasmi wa Everton kuanzia Julai 1 na amesaini Mkataba wa Miaka Mitatu.
Bosi wa Everton, Roberto Martinez, amesema anaamini  Deulofeu ana nafasi ya kukuwa na kuwa Mchezaji bora zaidi.
Deulofeu anakuwa Mchezaji wa Pili kusainiwa na Everton katika kipindi hiki baada ya kumpata Kiungo wa England Tom Cleverley aliejiunga kama Mchezaji Huru baada ya Mkataba wake na Manchester United kumalizika kufuatia kuichezea Aston Villa kwa Mkopo Msimu uliopita.
Nathaniel Clyne kujiunga Liverpool
Nathaniel Clyne yuko mbioni kujiunga na Liverpool baada ya Klabu yake Southampton kuikubali Ofa ya Pauni Milioni 12.5.
Clyne, ambae ni Fulbeki wa Kulia, anakuwa Mchezaji wa 6 kusainiwa na Liverpool katika kipindi hiki cha kuelekea Msimu mpya.
Uhamisho huu wa Clyne, mwenye Miaka 24 na ambae ameichezea England mara 5, utakamilika baada ya upimaji wa Afya yake na makubaliano ya maslahi yake binafsi.
Clyne atakuwa Mchezaji wa 4 kujiunga na Liverpool kutoka Southampton kufuatia wale waliojiunga Mwaka Jana ambao ni Adam Lallana, Dejan Lovren na Rickie Lambert.
SERGIO-RAMOS
Man United Mazungumzoni na Real kuhusu Sergio Ramos
Habari kutoka huko Spain zimedai kuwa Klabu za Manchester United na Real Madrid zipo kwenye mazungumzo kuhusu Uhamisho wa Sergio Ramos.
Vyanzo hivyo vinadai Man United imeshatoa Ofa ya Pauni Milioni 35 kumnunua Ramos lakini Klabu zote hizo mbili hazijasema lolote kuhusu hilo.
Ramos alisainiwa na Real Mwaka 2005 kutoka Sevilla kwa Dau la Euro Milioni 27 na amebakisha Miaka Miwili kwenye Mkataba wake wa sasa lakini hajapewa Ofa nyingine mpya na Real kitu ambacho kimemkera.

MSHIKEMSHIKE RAMOS NA REAL, ILA REAL YANG'ANG'ANIA LIPENI EURO MILIONI 200 MCHUKUENI!

1435127905 extras noticia foton 7 1Ile vita inayotokota kati ya Sergio Ramos na Klabu yake Real Madrid imeendelea na Leo hii Gazeti la Marca limeanika nini kiini chake cha kufikisha Beki huyo mahiri wa Spain kutaka kuhama na Manchester United ikitajwa ndiko aendako.
Migongano kati ya Rais wa Real, Florentino Pérez, na Sergio Ramos imekuwa mingi huku ikitajwa kwamba madai ya Mchezaji huyo ya kutaka kulipwa Pauni Milioni 10 kwa Mwaka baada ya kukatwa Kodi ni kitu hakikubaliki na kitu aina hiyo ndio kiliwakimbiza Mesut Özil na Ángel Di María hapo Santiago Bernabeu na kuangukia Arsenal na Manchester United ambako wanalipwa Dau kubwa kupita walipokuwa Real.
Lakini chanzo halisi cha mifarakano ya Ramos na Pérez kinaanzia wakati wa himaya ya Jose Mourinho wakati Beki huyo alipoongoza maasi ya kutaka Mourinho ang'olewe alipomzonga Rais Perez kwa kudai ama wao Wachezaji
wote au Mourinho mmoja lazima aondoke.
Hapo ndipo ufa mkubwa ukaanza kuonekana kati ya Perez na Ramos.
Hali hii imejidhihirisha hii Leo wakati Sergio Ramos na upande wake walipoenda kufanya mazungumzo rasmi na Real Madrid kwenye Kituo cha Real cha Mazoezi huko Valdebebas na badala ya kumkuta Rais Florentino Pérez wakaongea na Mkurugenzi Mtendaji José Ángel Sánchez.
Baada ya Mkutano huo, Ramos akaonekana akibeba vitu vyake binafsi toka hapo Valdebebas na kuondoka kitu ambacho kinaashiria kubaki kwake Real ni kitu kigumu.
Licha ya msuguano huu mkubwa, Bodi ya Real Madrid imekuwa ikisisitiza kuwa Sergio Ramos bado ana Mkataba wa Miaka Miwili na yeyote anaemtaka hivi sasa anapaswa kutimiza Kipengele cha Mkataba wake na kulipa Euro Milioni 200 ili wamwachie.

EURO U-21: PORTUGAL, SWEDEN ZATINGA NUSU FAINALI, ENGLAND, ITALY NJE!!


EUROU21Portugal na Sweden Jana zilitoka 1-1 kwenye Mechi ya Kundi ya Mashindano ya Nchi za Ulaya kwa Vijana chini ya Miaka 21, EURO U-21, huko Nchini Czech Republic na zote kutinga Nusu Fainali.
Matokeo hayo yameifanya Portugal iwe ya kwanza toka Kundi B na sasa watacheza na Germany na Sweden, waliochukua Nafasi ya PIli, watacheza na Denmark kwenye Nusu Fainali.
Katika Mechi hiyo, Portugal walipata Bao lao Dakika ya 82 kupitia Goncalo Paciencia na kama matokeo yangebaki hivyo basi Sweden wangetupwa nje kwa vile katika Mechi nyingine ya Kundi B, Italy walikuwa wakiifunga England.
Lakini DAkika ya 89 Simon Tibbling asliisawazishia Sweden na kuifikisha Nusu Fainali na kuacha ushindi wa 3-1 wa Italy dhidi ya England uwe bure kabisa.
Katika Mechi hiyo ya Italy na England, Italy walikuwa mbele 2-0 hadi Haftaimu kwa Bao za Belotti na Benassi ambae pia alipiga Bao la 3 Kipindi cha Pili huku Bao la England likifungwa Dakika ya 93 na Redmond.
VIKOSI:
England: Butland, Jenkinson, Stones, Gibson, Garbutt, Chalobah, Forster-Caskey, Redmond, Ings, Lingard, Kane.
Akiba: Bond, Ward-Prowse, Carroll, Keane, Afobe, Hughes, Moore, Chambers, Targett, Loftus-Cheek, Bettinelli.
Italy: Bardi, Zappacosta, Rugani, Romagnoli, Biraghi, Benassi, Crisetig, Cataldi, Berardi, Belotti, Trotta.
Akiba: Sportiello, Sabelli, VIviani, Bernardeschi, Barba, Bianchetti, Baselli, Izzo, Battocchio, Verdi, Leali.
REFA: Sergei Karasev (Russia).
MAKUNDI
KUNDI A
**Kila Timu imecheza Mechi 3
1 Denmark Pointi 6
2 Germany 5 
3 Czech Rep 4
4 Serbia 1
KUNDI B
**Kila Timu imecheza Mechi 3
1 Portugal Pointi 5
2 Sweden 4
3 Italy 4
4 England 3
****Timu 2 za juu za kila Kundi zitasonga Robo Fainali
RATIBA/MATOKEO:
**Mechi zote Saa 3 Dakika 45 Usiku
Jumapili Juni 21
Sweden 0 England 1
Italy 0 Portugal 0
Jumanne Juni 23
Czech Republic 1 Germany 1
Denmark 2 Serbia 0
Jumatano Juni 24
England 1 Italy 3
Portugal 1 Sweden 1
NUSU FAINALI
Jumamosi Juni 27
Demark v Sweden
Germany v Portugal
FAINALI
Jumanne Juni 30

Kikosi cha Atletico Madrid wameongeza nguvu kwa usajili wa kichwa kingine toka FC Porto

Jackson-Martinez
Siku chache baada ya kushuhudia mshambuliaji wake raia wa Croatia, Mario Mandzukic akihamia nchini Italia kwenye klabu ya Juventus, mabingwa wa Hispania kwa msimu wa mwaka 2013/2014 Atletico Madrid hii leo wamethibitisha kumsajili mshambuliaji raia wa Colombia Jackson Martinez toka FC Porto ya nchini Ureno.
Martinez amekuwa akitajwa kwenye vichwa vya habari za michezo akihusishwa na kujiunga na klabu kadhaa kubwa barani Ulaya ikiwemo Arsenal na AC Milan na kuna wakati iliaminika kuwa yuko karibu kujiunga na Ac Milan ambayo imekuwa ikisaka wachezaji wa kurudisha hadhi yake iliyopotea.
Mshambuliaji huyu mwenye umri wa miaka 28 amekuwa na rekodi nzuri ya ufungaji kwenye ligi ya Ureno tangu alipojiunga na FC Porto ambapo kwa misimu minne amefunga mabao 67 kwenye ligi huku msimu uliopita akifunga mabao 7 kwenye mechi 8 za michuano ya ligi ya mabingwa barani ulaya ambapo Porto ilifika hatua ya robo fainali .
jackson
Jackson Martinez
Martinez anakwenda Atletico Madrid kuziba pengo la mshambuliaji Mario Mandzukic ambaye amedumu kwenye klabu hiyo ya katikati ya mji mkuu wa Hispania kwa muda wa msimu mmoja tu tangu aliposajiliwa toka Bayern Munich ya Ujerumani.
Zaidi ya Hapo Martinez anafuata nyayo za mshambuliaji mwingine wa Colombia Radamel Falcao ambaye aliwahi kupita pia katika Kikosi cha Atletico Madrid kabla ya kujiunga na As Monaco na kisha Manchester United na hivi karibuni atajiunga na Chelsea ya England.


Real Madrid haitofata masharti ya Sergio Ramos? inabidi uijue hii

sergio-ramos-real-madrid_1hn6m16ku1c7w14s5iqq6i08yoKufuatia tetesi nyingi ambazo zimezidi kuongezeka miongoni mwa vyombo vya habari vya Hispania na England kuhusu mustakabali wa muda mrefu wa beki wa Hispania Sergio Ramos, uongozi wa klabu yake umeendelea kushikilia msimamo wake wa kutokuwekwa katika hali ya utata na beki huyo .
Uongozi wa rais Florentino Perez umesisitiza kuwa hautalazimika kutekeleza masharti ya beki huyo na badala yake atapaswa kuwa mtiifu kwa kuwa ana mkataba halali ambao lazima autumikie .
Sergio Ramos ameripotiwa kuwa karibu kuihama klabu hiyo baada ya kutoridhishwa na hali ya kutopewa ofa mpya wakati mkataba wake ukiwa umesaliwa na miaka miwili huku pia akihitaji kuongezewa mshahara .
Sergio 1Hadi sasa Ramos analipwa Euro Milioni 6 (zaidi ya BILIONI 15 ZA TANZANIA) kwa mwaka na anahitaji ongezeko la mpaka kufikia euro milioni 10 kwa mwaka baada ya makato ya kodi jambo ambalo Madrid wamesisitiza kuwa hawatalitekeleza.
Ripoti nyingine nchini England zimedai kuwa Ramos ametajwa kuwa kwenye orodha ya usajili ndani ya klabu ya Manchester United ambayo inataka kumtumia katika usajili wa David De Gea ambaye anatakiwa na Real Madrid .
United imewaambia Real kuwa kama wanamtaka De Gea basi wawe tayari kumuachia Ramos katika dili lolote la usajili wa kipa huyo hali ambayo imezua hofu miongoni mwa mashabiki wa Real Madrid .
SergioKatika misimu miwili iliyopita Real imewapoteza wachezaji wawili muhimu Angel Di Maria na Mesut Ozil ambao walikuwa wanadai nyongeza ya mshahara na matokeo yake walisajiliwa na timu za England.

Mambo Magugumu kwa Real Madrid na Sergio Ramos.

sergio-ramos-real-madrid_1hn6m16ku1c7w14s5iqq6i08yo

Kufuatia tetesi nyingi ambazo zimezidi kuongezeka miongoni mwa vyombo vya habari vya nchini Hispania na England kuhusu mustakabali wa muda mrefu wa beki wa Hispania Sergio Ramos uongozi wa klabu yake umeendelea kushikilia msimamo wake wa kutokuwekwa katika hali ya utata na beki huyo .
Uongozi wa rais Florentino Perez umesisitiza kuwa hautalazimika kutekeleza masharti ya beki huyo na badala yake atapaswa kuwa mtiifu kwa kuwa ana mkataba halali ambao lazima autumikie .
Sergio Ramos ameripotiwa kuwa karibu kuihama klabu hiyo baada ya kutoridhishwa na hali ya kutopewa ofa mpya wakati mkataba wake ukiwa umesaliwa na miaka miwili huku pia akihitaji kuongezewa mshahara .
Hadi sasa Ramos analipwa Euro Milioni 6 kwa mwaka na anahitaji ongezeko la mpaka kufikia euro milioni 10 kwa mwaka baada ya makato ya kodi jambo ambalo Madrid wamesisitiza kuwa hawatalitekeleza.
Ripoti nyingine nchini England zimedai kuwa Ramos ametajwa kuwa kwenye orodha ya usajili ndani ya klabu ya Manchester United ambayo inataka kumtumia katika usajili wa David De Gea ambaye anatakiwa na Real Madrid .
United imewaambia Real kuwa kama wanamtaka De Gea basi wawe tayari kumuachia Ramos katika dili lolote la usajili wa kipa huyo hali ambayo imezua hofu miongoni mwa mashabiki wa Real Madrid .
Katika misimu miwili iliyopita Real imewapoteza wachezaji wawili muhimu Angel Di Maria na Mesut Ozil ambao walikuwa wanadai nyongeza ya mshahara na matokeo yake walisajiliwa na timu za England .

Atletico Madrid wasajili mshambuliaji mpya .

Jackson-Martinez

Siku chache baada ya kushuhudia mshambuliaji wake raia wa Croatia Mario Mandzukic akihamia nchini Italia kwenye klabu ya Juventus , mabingwa wa Hispania kwa msimu wa mwaka 2013/2014 Atletico Madrid hii leo wamethibitisha kumsajili mshambuliaji raia wa Colombia Jackson Martinez toka Fc Porto ya nchini Ureno .
Martinez amekuwa akitajwa kwenye vichwa vya habari za michezo akihusishwa na kujiunga na klabu kadhaa kubwa barani ulaya ikiwemo Arsenal na Ac Milan na kuna wakati iliaminika kuwa yuko karibu kujiunga na Ac Milan ambayo imekuwa ikisaka wachezaji wa kurudisha hadhi yake iliyopotea .
Mshambuliaji huyu mwenye umri wa miaka 28 amekuwa na rekodi nzuri ya ufungaji kwenye ligi ya Ureno tangu alipojiunga na Fc Porto ambapo kwa misimu minne amefunga mabao 67 kwenye ligi huku msimu uliopita akifunga mabao 7 kwenye mechi 8 za michuano ya ligi ya mabingwa barani ulaya ambapo Porto ilifika hatua ya robo fainali .
Martinez anakwenda Atletico Madrid kuziba pengo la mshambuliaji Mario Mandzukic ambaye amedumu kwenye klabu hiyo ya katikati ya mji mkuu wa Hispania kwa muda wa msimu mmoja tu tangu aliposajiliwa toka Bayern Munich ya Ujerumani .
Zaidi ya Hapo Martinez anafuata nyayo za mshambuliaji mwingine wa Colombia Radamel Falcao ambaye aliwahi kupita Atletico Madrid kabla ya kujiunga na As Monaco na kisha Manchester United na hivi karibuni atajiunga na Chelsea ya England .

Cheki Mpira utakaotumiwa kwenye ligi ya England msimu ujao.

darren randolph new epl ball

Kukiwa kumesalia mizi miwili na siku kadhaa kabla ya ligi kuu ya England na lingi nyingine kubwa barani ulaya kuanza mpira rasmi utakaotumika kwenye ligi ya England umefahamika .
Mpira huo umebuniwa na kampuni ya vifaa vya michezo ya Kimarekani ya Nike ambapo utakuwa unafahamika kwa jina la Nike Ordem na umetengenezwa kwa kuzingatia teknolojia ya kisasa ambayo inaendana na mabadiliko ya mchezo wa soka .
Mpira huo umetengenezwa kwa kuzingatia jinsi ambavyo wachezaji watakuwa wakiutumia uwanjani ambapo moja ya vitu vilivyozingatiwa ni rangi yake na umetengenezwa kwa rangi angavu ili kuwasaidia wachezaji kuuona wakiwa uwanjani na kufanya maamuzi ya haraka.
Beki wa West Ham United  James Tomkins akiwa anaujaribu mpira mpya ambao utatumika kwenye msimu ujao wa ligi ya England .
Beki wa West Ham United James Tomkins akiwa anaujaribu mpira mpya ambao utatumika kwenye msimu ujao wa ligi ya England .
Mpira huo pia una sehemu 12 ambazo zinaufunika ili kuusaidia kwenda na kasi ambayo itawasaidia wachezaji wenye uwezo wa kupiga mashuti ya mbali .
Mpira huo ambao unatarajiwa kuzinduliwa mwezi julai pia utatumika kwenye ligi za Hispania na Italia na umeonekana ukifanyiwa majaribio na wachezaji wa klabu ya West Ham United kwenye uwanja wao wa mazoezi .
Winga wa West Ham Matt Jarvis akionekana akijaribu mpira huu ambao pia utatumika kwenye ligi za Hispania na Italia .
Winga wa West Ham Matt Jarvis akionekana akijaribu mpira huu ambao pia utatumika kwenye ligi za Hispania na Italia .

ALEXIS SANCHEZ AACHIA UJUMBE WA MAANA INSTAGRAM

29EF838600000578-3137813-image-a-42_1435164950127
Mshambuliaji wa Arsenal, Alexis Sanchez amewapa ujumbe mashabiki ambao wana matumaini ya kufikia ndoto zao.
Sanchez ame-post picha yake ya utotoni kwenye ukurasa wake wa Instagram inayoonesha kwamba alikuwa na ndoto ya kuwa mcheza soka.
The forward will play in the Copa America quarter final as Chile face Uruguay on Thursday
Amewaambia wafuasi wake “Usiruhusu mtu yeyote akaiba ndoto zako….endelea kupambana” .
Baada ya maneno hayo akatupia picha yake ya utotoni alipokuwa Buenos Aires.
Straika huyo alianza kucheza soka katika klabu ya Cobreloa ya Chile na sasa anaichezea Arsenal kutokea Barcelona, lakini aliwahi kukipiga Udinese

HILI NDO KINDA LA MIAKA 16 LILILODAKWA NA ARSENAL…

Screen-Shot-2015-06-24-at-10.42.52Arsenal wamemsajili nahodha wa timu ya taifa ya Romania ya vijana chini ya umri wa miaka 16, Vlad Dragomir, kwa muji wa shirika la habari la Reuters.
Kiungo huyo inasemekana amekataa kujiunga na mabingwa wa Romania Steaua Bucharest na kwenda Arsenal akitokea ACS Poli Timisoara.
“Nimefurahi sana,ni matumaini yangu kuwa sijamkasirisha yeyote. Niliona nafasi ya kwenda Arsenal ni nzuri kwangu, nahisi hapo ndio mahala pangu”, amesema.

TETESI ZA USAJILI ULAYA ZILIZO TAMBA LEO….

Di MariaWinga wa Manchester United Angel Di Maria, 27, anasakwa na Barcelona (Sport).
Matumaini ya Arsenal kumsajili Jackson Martinez, 28, kutoka Porto yamekwisha baada ya mchezaji huyo kutoka Colombia kusaini mkataba wa miaka minne Atletico Madrid (AS).
Manchester United wanamtaka Sergio Ramos ili kubadilishana na David De Gea. Real Madrid wanamtaka De Gea, 24, pamoja na pauni milioni 20 za kumnunua Ramos. Utd watamzuia De Gea kuondoka iwapo Real watakataa mpango huo (Daily Star).
West Ham hawatomuuza Andy Carroll msimu huu (Sun).
Newcastle wapo katika nafasi kubwa ya kumsajili Charlie Austin, 25 kwa pauni milioni 14. Mchezaji huyo anatakiwa na Southampton, Chelsea na West Ham (Daily Express)
Newcastle na Stoke wanamtaka winga kutoka Ukraine Yevhen Konoplyanka ambaye atakuwa mchezaji huru baada ya mkataba wake kukamilika na Dnipro (Daily Mirror).
Stoke City wanatarajia dau la pauni milioni 8 kutoka Chelsea kumchukua kipa Asmir Begovic, 28, na watataka Victor Moses kuunganishwa katika mkataba huo (Daily Telegraph).
Hata hivyo matumaini ya Chelsea yana wasiwasi baada ya Moses, 24, kusema hana uhakika kama anataka kurejea Stoke alipocheza kwa mkopo msimu uliopita Times).
West Brom wanajiandaa kumfanya Demba Ba, 30, mchezaji anayelipwa zaidi (Birmingham Mail)
West Ham wamekubali mkataba wa pauni milioni 12 kumsajili kiungo wa Marseille Dimitri Payet, 28 (Daily Mail).
Rais wa zamani wa Real Madrid, Ramon Calderon amesema Manchester United watakuwa na “bahati sana” kumsajili Sergio Ramos, 29 (TalkSport).
Meneja wa Tottenham Mauricio Pochettino ana matumaini ya kuwashawishi wachezaji wake muhimu, kwa kumfaya kipa Hugo Lloris, 28, kuwa nahodha na Harry Kane, 21, kuwa naibu nahodha (Daily Mirror).
Winga wa Chelsea Mohamed Salah, 23, anatarajiwa kuwaambia Fiorentina kama atasalia Italia au la, baada ya kuichezea klabu hiyo kwa mkopo msimu uliopita (Daily Telegraph).
Sunderland wametoa dau la zaidi ya pauni milioni 11 kumchukua kiungo wa PSV Eindhoven Georginio Wijnaldum, 24, ambaye anasakwa pia na Newcastle (Guardian).
Manchester United wameacha kumfuatilia Ilkay Gundogan ambaye huenda akasalia Borussia Dortmund wakati Utd wakitafuta kuingo kwingineko (Daily Star)
Uhamisho uliothibitishwa nitakujulisha.