tecno

tecno

airtel

airtel

.

.

nido

nido

RADIO LISTEN NOW

3 Julai 2015

LIGI KUU ENGLAND: MECHI YA MAN UNITED NA VILLA KUCHEZWA IJUMAA USIKU!

BPL-2014-2015-LOGO-POAMechi ya Manchester United na Aston Villa, ambayo ni Mechi ya Pili ya Ligi Kuu England kwa Timu hizo kwa Msimu mpya wa 2015/16, itachezwa Ijumaa Usiku.
Mechi hiyo ambayo ilikuwa ichezwe Villa Park Jumamosi Agosti 15 imerudishwa nyuma na sasa itachezwa Ijumaa Agosti 14 kutokana na eneo hilo kuwa na maandamano Siku hiyo ya Jumamosi.
Pia, kwa sababu Man United watakuwa na Mechi ya UEFA CHAMPIONZ LIGI hapo Jumanne Agosti 18, Mechi hiyo imeshindikana kupangwa Jumapili Agosti 16.
Mechi hii ya Ijumaa Usiku itarushwa moja kwa moja huko England na Kituo cha TV cha Sky Sports kuanzia Saa 3 Dakika 45 Usiku, Saa za Afrika Mashariki.
Wasimamizi wa LIgi Kuu England wamesema walipaswa kuiondoa Mechi hii kuchezwa Jumamosi kutokana na ushauri wa Polisi kutokana na Maandamano hayo.
Si kawaida kwa Mechi za Ligi Kuu England kuchezwa Ijumaa ingawa tayari ipo mipango iliyopitishwa pamoja na Vituo vya TV kwamba katika Msimu wa 2016/17 Mechi 10 za Ligi hiyo zichezwe Ijumaa Usiku.

Breaking News: Baada ya kuondoka Man Utd, Falcao arudi tena kucheza EPL

Miezi takribani miwili baada ya klabu ya Manchester United kuamua kutoendelea kupokea huduma za Radamel Falcao kwa kutompa mkataba wa kudumu, mchezaji huyo wa Colombia amepata timu mpya ndani ya ligi kuu ya Uingereza. 
Falcao ambaye ni nahodha wa timu ya taifa ya Colombia, anatarajia kujiunga na Chelsea kutokea Monaco kwa mkataba wa mwaka mmoja wa mkopo.
Mchezaji huyo msimu uliopita alisajiliwa na Manchester United kwa mkopo wa mwaka mmoja na endapo angewaridhisha benchi la ufundi la klabu hiyo kwa kiwango kizuri basi angesajiliwa kwa mkataba wa kudumu, hata hivyo hakufanikiwa kumshawishi Louis Van Gaal kumpa mkataba huo.
  Sasa anajiunga na Jose Mourinho, kocha ambaye amekuwa hafichi mapenzi yake mbele ya mchezaji huyo ambaye alijaribu kumsajili kwa muda mrefu bila mafanikio.

ASILIMIA 55 YA MASHABIKI WA REAL MADRID WANATAKA RAMOS ASEPE

ramos
Labda ni tofauti na vile ilivyotegemewa jinsi mashabiki wa Real Madrid wangelichukulia hili swala la Ramos kutaka kusepa kwenye club yao.
Labda wangembembeleza kubaki lakini kutokana na survey iliyofanyw na gazeti maarufu la michecho la huko Huspania (AS) limetoa ripoti kwamba 55% ya mashabiki wa Real Madrid wanataka mchezaji huyo asepe kwenye hiyo club. Wakati 45% tu ndio wanataka abaki.
Real Madrid kwa sasa wamesema hawata muuza Ramos kwa gharama ya chini ya €90 million. Survey nyingine ya gazeti la A.S imetoa majibu kuhusu utata wa thamani ya mchezaji huyu, asilimia 22 ya mashabiki wa Real Madrid wamesema kwamba Ramos asiuzwe kwenye club yoyote ya EPL chini ya €60m

KOMBE LA DUNIA WANAWAKE: MAMBO MUHIMU JAPAN IKIIFUNGA UINGEREZA NA KUTINGA FAINALI

JAPAN
Simon Chimbo;
Katika kipindi chote hiki cha kombe la dunia la wanawake shaffihdauda.co.tz imeendelea kukuletea tathimini ya michezo mbalimbali inavyoondelea. Katika mchezo wa nusu fainali kati ya Japan na Uingereza haya ndio yaliyojiri:
  • Japan wameifunga Uingereza 2-1 na kutinga fainali kwa mara ya pili mfululizo. Japan imekua ni timu ya pili kutetea ama kucheza fainali wakiwa ndio mabingwa watetezi, wakiwalipa Ujerumani walipokuwa mabingwa 2003 na kucheza tena 2007.
  • Japan ni nchi ya nne kucheza fainali mara mbili mfululizo, wakiwafuata Marekani, Ujerumani na Norway.
  • Japan imefunga goli la kwanza katika mechi zote sita ilizocheza msimu huu wa kombe la dunia na pia imeshinda michezo yote sita. Ushindi wote wa Japan katika michezo hiyo sita umekuwa ni wa tofauti ya goli moja.
  • Aya Miyama wa Japan alifunga kwa penati goli lake la sita na kuwa wa pili nyuma ya Homare Sawa mwenye magoli nane ya kombe la dunia katika historia ya Japan.
  • Mchezaji Fara Williams wa Uingereza alifunga kwa penati na kufikisha magoli manne tangu acheze kombe la dunia na kumfikia Kelly Smith katika rekodi ya ufungaji bora wa muda wote wa kombe la dunia la wanawake kwa Uingereza.
  • Uingereza walifungwa pamoja na kuwa na mashuti mengi golini 15-7 dhidi ya Japan, na pia waligusa mpira mara nyingi katika eneo la penati la Japan mara 24-18 dhidi ya Japan.
Mchezo wa fainali:
  • Marekani itacheza na Japan katika mchezo wa fainali ya kisasi katika mechi itakayo pigwa mjini Vancouver baada ya ushindi wa matuta wa Japan 2011 walipotoshana nguvu kwa mabao 2-2 fainali.
  • Hii ni fainali kubwa ya tatu kuwakutanisha Japan na Marekani. Marekani iliwafunga Japan magoli 2-1 katika fainali za Olimpiki 2012.
  • Kila timu imefunga mara tisa katika michezo sita kwenye fainali za mwaka huu zinazoendelea huku Marekani wakiruhusu goli moja pungufu ya Japan.
  • Japan wanaongoza kwa kupiga pasi nyingi, 80% ukilinganisha na 74% za Marekani.
Hayo ndiyo yaliyojiri katika hatua hii ya nusu fainali, usikose mchezo wa fainali siku ya Jumapili kati ya Marekani na Japan.

MAKALA : KWANINI TIMU HAZITUMII PESA NYINGI KUSAJILI MABEKI

LOGO
Simon Chimbo;
Mwezi Juni hadi Agosti ni miezi nyeti katika soka na hususan kwa wale mashabiki wa ligi kubwa tano duniani. Miezi hii ni kipindi ambacho timu, mashabiki pamoja na vyombo vya habari huwa macho kujua nani anakwenda wapi na nani wanamhitaji.
Lakini swali hapa ni kwamba, kwanini ni ngumu kukuta katika picha za nje za magazeti kipindi hiki cha usajili kuna sura za mabeki?
Mfano angalia ambavyo jina la Raheem Sterling, Harry Kane, Paul Pogba na washambuliaji wengine yalivyotawala katika magazeti ya michezo? Kwanini hatuoni mabeki? Ukiachilia mbali mlinzi wa Real Madrid, Sergio Ramos na golikipa David de Gea wa Manchester United, bado hata bei zao hazitajwi kuwa kubwa.
Sio kwamba walinzi hawasajiliwi, la hasha! Ila hawana thamani hii wanayopewa akina Paul Pogba na Raheem Sterling.
Kumbe mwisho wa haya yote tunapata jibu kwamba kumbe soka ni mchezo wa matokeo. Ndio maana Liverpool wamemsajili mlinzi chipukizi wa Southampton Nathael Clyne kwa pauni 12m huku wakimsajili mshambuliaji wa brazil Roberto Firmino kwa pauni 29m.
Leo hii klabu ya Manchester United hawako tayari kutoa zaidi ya pauni 35m kwa mlinzi wa kati wa Real Madrid, Sergio Ramos lakini usishangazwe wakitoa pauni 75m kwa mshambuliaji Gareth Bale wa klabu hiyo hiyo ya Madrid.
Mpira ni mchezo wa ushindi, yaani magoli. Ndio maana sijashtushwa na usajili wa pauni 12m wa mlinzi mbrazil kutoka Atletico Madrid, Miranda wa kwenda Inter lakini nitashangaa kuona mshambuliaji wao Arda Turan akiuzwa kwa pungufu ya pauni 25m.
Kimsingi hapa ni namna mfumo wa mpira unavyobadilika, katika ‘modern game’ walinzi wamebadilishiwa majukumu na kwamba siku hizi mashambulizi ya timu huanzia kwa mabeki. Walinzi wa pembeni siku hizi wamekuwa na kazi ndogo zaidi ya ulinzi kuliko kushambulia kutokea pembeni.
Mlinzi Dany Alvez ameonekana mara nyingi katika nusu ya pili ya eneo pinzani awapo uwanjani, lakini hali hiyo utaikuta pia kwa Philip Lahm wa Ujerumani. Mpira ni magoli, ni ushindi. Ndio maana Barcelona walitoa pauni 75m kumsajili Luis Suarez lakini kamwe hawawezi kutoa hata pauni 50m kumsajili mlinzi Diego Godin ama Vicent Kompany.
Hizo pamoja na sababu nyingine za matangazo ya kibiashara hufanya timu kutoa macho zaidi kuwanunua wachezaji wa kiungo na ushambuliaji kwa ada kubwa zaidi ya mabeki.
Thamani ya watu wa ulinzi inashuka na pengine ndio maana Sepp Blatter alimpa tuzo ya mchezaji bora wa dunia Cannavaro wa Italia mwaka 2006 ili kujaribu kuinua thamani yao katika mchezo wa soka.
Pengine watu watasema hii ni Ulaya tu? Hapana ni kila sehemu ya dunia hivi sasa. Kwani hatuoni magazeti yetu ya hapa bongo? Vichwa vya nje vimepambwa majina ya akina Kaseke, Okwi, Busungu na Niyonzima, lakini kwanini sio Oscar Joshua? Mpira ni magori, ushindi.

TERRY AONESHA KABATI LA MAKOMBE ALIYOWAHI KUTWAA

TerryWakati ligi nyingi Ulaya zikiwa zimemalizika na wachezaji wakiwa kwenye mapumziko, nahodha wa Chelsea John Terry ameitumia likizo yake kuonesha mafanikio aliyoyapata toka aanze kucheza mchezo wa soka mpaka leo.
Beki huyo wa kati aliposti picha kwenye mtandao wake  wa Instagram ya makombe ambayo amewahi kushinda, huku kombe la ligi kuu England likiwa ndiyo kombe ambalo ametwaa hivi karibuni akikiongoza kikosi cha Chelsea.
Terry 1Hakitakuwa kitu cha kushangaza kama Terry, 34, atatwaa taji jingine msimu ujao wa ligi ambayo inatarajiwa kuanza Agosti 8 huku Chelsea ikianzia nyumbani Stamford Bridge dhidi ya Swansea City.
Mataji yote manne ya EPL yameonekana kwenye kabati lake, kombe la klabu bingwa Ulaya ambalo Chelsea walishinda 2012 kwa kuifunga Bayern Munich kwa mikwaju ya penati. Vikombe vingine ni pamoja na makombe matano ya FA, makombe matatu ya ligi na kombe moja la Europa Legue.
Ingawa Terry hakucheza kwenye fainali ya Uefa baada ya kulimwa kadi nyekundu kwenye mchezo wa nusu fainali kufutia kumfanyia rafu Alexis Sanchez wakati Chelsea ikicheza na FC Barcelona.
Terry 2Lakini hio bado haikumzuia nahodha huyo wa kikosi cha Chelsea kujumuika na timu nzima kuendeleza sherehe kwenye dimba la Allianz Arena.
Kitendo hicho kilikosolewa sana na watu wengi lakini Terry alijitetea akiliambia gazeti la Dily Tlegraph: “Ulikuwa ni usiku mkubwa kuwahi kutokea kwa klabu nzima na mimi sikucheza. Nilijihisi ni sehemu ya  waliocheza, waliocheza walinifanya nijihisi ni sehemu yao. Ukitazama nyuma, kwenye mechi dhidi ya Napoli (hatua ya 16 bora) na michezo mingine ambayo nilitoa mchango wangu mkubwa sana”.
Kwa ujumla, Terry ameshashinda mataji 14 akiwa na klabu yake ya Chelsea ambayo alianza kucheza tangu akiwa mdogo.

ARSENAL KUMPATA MMOJA KUUZA WANNE, GUEYE AENDA VILLA, DE GEA ATUA MADRID....!!

soc-portugals-william-carvalho-and-swedens-oscar-lewicki-in-actionLeo zimeibuka ripoti kuwa Arsenal itamchukua Mchezaji mmoja kutoka Ureno na kuuza Wanne huku Aston Villa ikiwa njiani kumpata Kiungo wa Senegal wakati Kipa wa Manchester United, David de Gea, akionekana huko Barajas, Uwanja wa Ndege wa Jiji la Madrid.
ARSENAL
Baada ya kumnunua Kipa wa Chelsea, Petr Cech, Meneja Arsene Wenger, sasa yupo karibu kumchukua Kiungo William Carvalho kutoka Sporting Lisbon ya Ureno.
Carvalho alikuwa mmoja wa Nyota wa Ureno waliong'ara hivi Juzi huko Czech Republic kwenye Fainali za EURO U-21 ambako Timu yao ilifungwa Fainali na Sweden kwa Penati 4-3.
Wakati Wenger akisaka wapya na baada ya kumtema Abou Diaby, Wachezaji wengine Wanne wanapelekwa Sokoni kwani Arsenal haiwataki tena na hao ni David Ospina, Lukas Podolski, Mathieu Flamini na Joel Campbell.
Nae Mikel Arteta atapewa nyongeza ya Mwaka mmoja katika Mkataba wake.
ASTON VILLA
Aston Villa wako njiani kumsaini Kiungo wa Lille ya Ufaransa Idrissa Gueye kwa Dau la Pauni Milioni 9.
Tayari Gueye, Mchezaji wa Kimataifa wa Senegal mwenye Miaka 25, yupo Mjini Birmingham kukamilisha Dili hii.
Ikiwa Gueye atasainiwa atakuwa Mchezaji wa 3 kwa Meneja Tim Sherwood kwa kipindi hiki na wengine ni Beki wa Man City Micah Richards na Fowadi Scott Sinclair.
Gueye ameichezea Lille Mechi 134 na mara 18 kwa Timu ya Taifa ya Senegal.
David-de-Gea-shangilia
DAVI DE GEA
Huku ikiaminika Kipa wa Manchester United David de Gea atarudi kwao kuidakia Real Madrid, Kipa huyo Leo alinaswa akitua Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Barajas uliopo Jijini Madrid.
Kipa huyo anatakiwa Jumatatu aripoti huko Carrington Jijini Manchester kwa ajili ya kuanza Mazoezi kwa ajili ya Msimu mpya na Ziara ya Man United huko USA ambayo Timu hiyo itasafiri Julai 14.
Akiwa Uwanjani hapo, De Gea alisisitiza yuko Madrid kwa mapumziko tu.
Inadaiwa hivi sasa Man United ishanyoosha mikono kwa Real kumchukua De Gea lakini si Bei ya kutupwa bali kwa Dau nono na ikiwa hilo haliwezekani basi wao wako tayari kumbakisha Old Trafford hadi Mkataba wake utakapoisha Mwakani.

WEST HAM YAANZA VYEMA SAFARI NDEFU YA EUROPA LIGI, YAPIGA 3!

EUROPALIGI-NICE-2West Ham wameanza safari ndefu ya kufuzu kucheza Makundi ya UEFA EUROPA LIGI kwa kuichapa Lusitanos ya Andorra Bao 3-0 katika Mechi ya Kwanza ya Raundi ya Kwanza ya Mtoano iliyochezwa Jana Usiku huko Upton Park Jijini London.
Mechi hii ilikuwa ni moja ya Mechi 51 za Kwanza za Raundi ya Kwanza ya Mtoano zilizochezwa Jana Usiku.
Timu hizi zitarudiana Julai 9 huko Andorra na Mshindi atatinga Raundi ya  Pili ya Mtoano na kucheza na Mshindi kati ya Birkirkara FC ya Malta na Ulisses FC ya Armenia.
Bao za West Ham katika Mechi hii na Lusitanos zilifungwa na Diafra Sakho, Bao 2 katika Kipindi cha Kwanza, na James Tomkins.
West Ham walicheza Mechi hii wakishuhudiwa na Watazamaji 35,000 pamoja na Meneja wao mpya Slaven Bilic wakati Timu ikisimamiwa na Kocha wa Vijana, Terry Westley.
West Ham, ambao walimaliza Ligi Kuu England Nafasi ya 12, wamefuzu kucheza EUROPA LIGI kwa Tiketi ya Uchezaji wa Haki [Fair Play] kwa sababu wao walikuwa juu kwenye Tebo yake kwa Timu za Ligi Kuu England.
Timu nyingine za England ambazo zitashiriki EUROPA LIGI ni Liverpool na Tottenham zilizomaliza Ligi Kuu England zikiwa Nafasi za 6 na 7 lakini wao wataanzia Hatua ya Makundi.
Ili West Ham wafike Makundi, inabidi wavuke Raundi 4 za Mtoano.

CHICHARITO AFANYIWA OPERESHENI, SASA HAUZIKI!

78dd3b3a-bfb9-4e68-b91e-408088e4a9ef-2060x1236Straika wa Mexico Javier Hernández 'Chicharito' amevunjika mfupa wa begani na kufanyiwa operesheni ambayo itamweka nje kwa Wiki 4 na kukosa kuichezea Nchi yake Mashindano ya CONCACAF Gold Cup.
Chicharito aliumia Jumatano iliyopita huko Houston, USA wakati wa Mechi ya Kirafiki na Honduras iliyoisha 0-0 na kutolewa nje Dakika 5 kabla Haftaimu.
Msimu uliopita, Chicharito, mwenye Miaka 27 na ambae ni Fowadi wa Manchester United, alikuwa na Real Madrid kwa Mkopo na alipaswa kurudi Old Trafford huku kukiwa na fununu za mipango ya kumuuza.
Lakini kuumia kwake na kufanyiwa operesheni iliyomwekea chuma kwenye mfupa wa begani kutamweka nje kwa Wiki 4 na hali hii itafanya mipango hiyo ya Uhamisho wake isitishwe.
Kukosekana kwa Chicharito pia ni pigo kwa Mexico kwani ni Mfungaji wa Bao 40 katika Mechi 73 za Nchi hiyo na walimtegemea sana kwenye Mashindano ya CONCACAF Gold Cup ambalo ni Kombe la Mataifa ya Nchi za Marekani ya Kaskazini, ya Kati na Visiwa vya Carribean yakatayochezwa Julai 7 hadi 26 huko Canada na United States.
Mexico wako Kundi C na wataanza kwa kucheza na Cuba hapo Julai 9 huko Chicago kisha kuzivaa Guatemala na Trinidad and Tobago.
Kocha wa Mexico Miguel Herrera amemwita Javier Orozco wa Klabu Bingwa ya Mexico Santos Laguna kumbadili Chicharito.

NANI KUTUA KUKIPIGA KLABU HII HAPA…..

Nani 2Winga wa Manchester United Luis Nani Jumapili atatua Instanbul kwa ajili ya kukamilisha vipimo vya afya kwa ajili ya kujiunga na klabu ya Fenerbahce ya Uturuki.
Taarifa kutoka Fenerbahce imethibitisha: “Fenerbahce imefungua majadiliano na  Luis Nani na klabu yake ya Manchester United kwa ajili ya kumsajili mchezaji huyo”.
Nani“Kuanzia Jumapili Nani atakuwa Istanbul kwa ajili ya kufanyiwa vipimo vya afya”.
Mchezaji huyo wa kimataifa wa Ureno, alisaini mkataba wa miaka mitano mwaka 2013 kuitumkia United wakati David Moyes alipokuwa kocha wa Manchester.
Lakini baada ya kocha huyo kutimuliwa, nafai ya Nani ilikuwa ndogo kwenye kikosi cha Old Trafford hasa pale alipotua kocha mpya Louis van Gaal ambaye alionekana hana mipango ya baadae na Nani.
Nani 1Msimu uliomalizika wa 2014-2015 nani alitolewa kwa mkopo na alikipiga kwenye klabu ya nymbani kwao (Ureno) Sporting Lisbon.

DE GEA ATIMKIA MADRID, KISA NINI…SABABU ZOTE ZIKO HAPA

De GeaGolikipa wa Manchester United David de Gea amesafiri kuelekea jijini Madrid kwa ajili ya mapumziko ya mwishoni mwa msimu, mashabiki wa Man United wanaweza wakawa hawajafurahia kipa huyo kutimkia Madrid kwa kuhofia huenda akawa anataka kufanikisha dili la kuhamia kwenye klabu ya Real Madrid lakini yeye De Gea amsema ameamua kwenda nyumbani kwao kwa ajili ya likizo.
“Nipo mapumzikoni (likizo) na kila kitu kinakwenda sawa”.
De Gea 1De Gea ambaye bado anamkata wa mwaka mmoja wa kuendelea kusalia Old Trafford, anatarajia kujiunga na Real Madrid wakati huu wa usajili wa majira ya joto.
Mashetani Wekundu wako tayari kupokea ofa kutoka Real Madrid kwa ajili ya De Gea na wataendelea kuweka msimamo wa kumuuza kwa dau la pauni milioni 35 kwa ajili ya ada yake ya uhamisho.
Man United wako tayari kumlipa De Gea kitita cha pauni 200,000 kwa wiki lakini golikipa huyo mwenye miaka 24 anaonekana anataka kurejea nyumabani kwao Madrid.
De Gea 2Gazeti la Sportmail la wiki iliyopita liliripoti kuwa, uongozi wa United huenda ukaamua kumshikilia De Gea kwa miezi 12 iliyobaki kwenye mkataba wake kuliko kupokea ofa ambayo itakuwa ndogo na haina faida kwao.
Wanaamini mlindamlango huyo mzaliwa wa Real Madrid anathamani ya pauni milioni 35 na hio ndiyo ofa pekee ambayo wanaweza kuikubali ambayo huenda ikavunja rekodi kwa uhamisho wa golikipa.
De Gea 3De Gea aliyejiunga na Manchester United akitokea Atleico Madrid ambao ni wapinzani wa jadi wa Real Madrid mwaka 2011, anawavutia magwiji hao wa Santiago Bernabeu baada ya kuonesha kiwango cha juu kwenye msimu mwingine uliomalizika hivi karibuni.