tecno

tecno

airtel

airtel

.

.

nido

nido

RADIO LISTEN NOW

18 Aprili 2016

WENGER AKATA TAMAA UBINGWA AHIMIZA VITA KUBAKI 4 BORA!

WENGER-PALACEBAADA ya Jana kutoka Sare 1-1 na Crystal Palace kwenye Mechi ya BPL, Ligi Kuu England, Meneja wa Arsenal Arsene Wenger amekata tamaa kutwaa BPL-APR17Ubingwa na kusisitiza mkazo wa kumaliza Ligi ndani ya 4 Bora.
Matokeo ya Jana yamewaacha Arsenal wakiwa Nafasi ya 4 kwenye BPL wakiwa nyuma ya Timu ya 3 Man City kwa tofauti ya Magoli na wakiwa Pointi 13 nyuma ya Vinara Leicester City huku wao wakibakisha Mechi 5.
Nyuma ya Arsenal zipo Man United na West Ham ambazo nazo zina matumaini ya kuingia 4 Bora na kuinyima Timu ya Wenger kumaliza ndani ya 4 Bora kwa mara ya 20 mfululizo.
Baada ya Mechi hiyo na Palace, Wenger aliongea: "Ukweli baada ya Gemu ya Lei sipo kwenye hali njema kuongelea kutwaa Ubingwa. Nipo kwenye hali ya kuitengeneza Timu kiakili kwa ajili ya Mechi ijayo Alhamisi na West Brom. Ni muhimu kuzitazama Timu za nyuma yetu kwani zinacheza vizuri na zinashinda!"
Aliongeza: "Kwetu tunapaswa kupigana hadi mwisho ili tuwemo 4 Bora!"
LIGI KUU ENGLAND
Ratiba:
Jumatatu Aprili 18
2200 Stoke v Tottenham             
Jumanne Aprili 19
2145 Newcastle v Man City         
Jumatano Aprili 20
2145 West Ham v Watford          
2200 Liverpool v Everton            
2200 Man United v Crystal Palace          
Alhamisi Aprili 21
2145 Arsenal v West Brom          
Jumamosi Aprili 23
1445 Man City v Stoke
1700 Aston Villa v Southampton           
1700 Bournemouth v Chelsea               
1700 Liverpool v Newcastle                  
Jumapili Aprili 24
1605 Sunderland v Arsenal         
1815 Leicester v Swansea 
Jumatatu Aprili 25
2200 Tottenham v West Brom   

Hakuna maoni: