2 ZA 4 BORA KATI YA CITY, LIVERPOOL NA ARSENAL KUAMULIWA SIKU YA MWISHO JUMAPILI!
WAKATI
Mabingwa wapya Chelsea na Tottenham Hotspur tayari zishakata Tiketi 2
za Timu 4 Bora za EPL, LIGI KUU ENGLAND, vita imebaki 2 zipi za mwisho
zitaungana nao.
Hapo Jumapili Arsenal kwanza inapaswa kuifunga Timu ya 7 Everton na pia kuomba Liverpool inafungwa na Middlesbrough ambayo tayari ishashuka Daraja.
ARSENAL KUMALIZA 4 BORA - LAZIMA:
-Washinde na Liverpool ishindwe kuifunga Boro.
-Watoke Sare 0-0 au 1-1 na Liverpool kwa Bao 3 au zaidi.
-Wapate Sare ya Magoli ya 2-2 na Liverpool wafungwe 2-0 au Sare 3-3 na Liverpool wafungwe 3-1 na kadhalika.
-Washinde na Man City wafungwe na kubadili tofauti ya Magoli.na kuwa zaidi ya 5.
LIVERPOOL WATAMALIZA 4 BORA IKIWA:
-Watashinda au watapata matokeo yeyote bora kupita Arsenal
EPL, LIGI KUU ENGLAND
Ratiba/Matokeo:
Jumatatu Mei 15
Chelsea 4 Watford 3
Jumanne Mei 16
Arsenal 2 Sunderland 0
Manchester City 3 West Bromwich Albion 1
Jumatano Mei 17
2145 Southampton v Manchester United
Alhamisi Mei 18
2145 Leicester City v Tottenham Hotspur
Jumapili Mei 21
Mechi za Mwisho za Ligi, zote kuanza Saa 11 Jioni
Arsenal v Everton
Burnley v West Ham United
Chelsea v Sunderland
Hull City v Tottenham Hotspur
Leicester City v Bournemouth
Liverpool v Middlesbrough
Manchester United v Crystal Palace
Southampton v Stoke City
Swansea City v West Bromwich Albion Watford v Manchester City
Vita
hiyo sasa imebaki kwa Liverpool, Man City na Arsenal ambayo itaamuliwa
kwenye Mechi za mwisho za Msimu hapo Jumapili Mei 21 baada Jana Man City
na Arsenal zote kushinda Mechi zao za Kiporo.
Jana
Man City wakiwa kwao Etihad waliitandika West Bromwich Albion 3-1 huku
Bao zao zikipigwa na Gabriel Jesus, Dakika ya 27, Kevin De Bruyne, 29,
na Yaya Toure, 57.
Bao la WBA lilifungwa na Robson-Kanu Dakika ya 87.
Kwenye Mechi yao ya mwisho hapo Jumapili Ugenini na Watford, Man City wanahitaji Sare tu ili kujihakikishia kuwemo 4 Bora.
Huko
Emirates Jijini London, Arsenal waliifunga Timu ambayo tayari
ilishashushwa Daraja Sunderland Bao 2-0 zote zikifungwa Kipindi cha Pili
na Alexis Sanchez na kujiwekea matumaini ya kufuzu 4 Bora ikiwa mambo
kadhaa yatatokea hapo Jumapili kwenye Mechi za mwisho kabisa za Ligi.
Hapo Jumapili Arsenal kwanza inapaswa kuifunga Timu ya 7 Everton na pia kuomba Liverpool inafungwa na Middlesbrough ambayo tayari ishashuka Daraja.
Arsenal wapo Nafasi ya 5 wakiwa Pointi 1 nyuma ya Liverpool ambao pia wana Goli 2 zaidi katika Tofauti ya Magoli.
-Washinde na Liverpool ishindwe kuifunga Boro.
-Watoke Sare 0-0 au 1-1 na Liverpool kwa Bao 3 au zaidi.
-Wapate Sare ya Magoli ya 2-2 na Liverpool wafungwe 2-0 au Sare 3-3 na Liverpool wafungwe 3-1 na kadhalika.
-Washinde na Man City wafungwe na kubadili tofauti ya Magoli.na kuwa zaidi ya 5.
LIVERPOOL WATAMALIZA 4 BORA IKIWA:
-Watashinda au watapata matokeo yeyote bora kupita Arsenal
EPL, LIGI KUU ENGLAND
Ratiba/Matokeo:
Jumatatu Mei 15
Chelsea 4 Watford 3
Jumanne Mei 16
Arsenal 2 Sunderland 0
Manchester City 3 West Bromwich Albion 1
Jumatano Mei 17
2145 Southampton v Manchester United
Alhamisi Mei 18
2145 Leicester City v Tottenham Hotspur
Jumapili Mei 21
Mechi za Mwisho za Ligi, zote kuanza Saa 11 Jioni
Arsenal v Everton
Burnley v West Ham United
Chelsea v Sunderland
Hull City v Tottenham Hotspur
Leicester City v Bournemouth
Liverpool v Middlesbrough
Manchester United v Crystal Palace
Southampton v Stoke City
Swansea City v West Bromwich Albion Watford v Manchester City
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni