tecno

tecno

airtel

airtel

.

.

nido

nido

RADIO LISTEN NOW

29 Mei 2017

Hivi unajua?kutapigwa El Classico 3 kabla ya msimu kuanza.

Ni fainali ya Champions League tu ndio imebaki ili kukamilisha michezo yote ya msimu wa 2016/2017 kwani tayari karibia ligi zote kuu zimemalizika.

Lakini jambo la faraja kwa mashabiki wa soka ni kwamba pambano la kati ya Real Madrid na Barcelona (El Classico) litapigwa mara tatu kabla hata ya msimu ujao wa ligi kuanza.

Kushinda kwa Barcelona kombe la Copa Del Rey kunamaanisha timu hizo mbili zitachuana katika mchezo wa Spanish Super Cup ambayo kwa kawaida huchezwa mara mbili nyumbani na ugenini.

Lakini bado tena mwezi wa July tarehe 28 mjini Miami Florida wababe hao watakutana katika fainali ya International Champions Cup hiyo nayo ikiwa ni bado ligi haijaanza.

Habari hii inaweza kuwa faraja kwa wapenzi wengi wa soka kwani ligi kwenda mapumzikoni zimefanya furaha ya wapenda soka kupungua kwa kiasi kikubwa.

Hakuna maoni: