tecno

tecno

airtel

airtel

.

.

nido

nido

RADIO LISTEN NOW

30 Juni 2015

BAADA KUTUPWA NJE, DUNGA ADAI COPA AMERICA HAINA 'MAANA YEYOTE!'

DUNGA-BRAKocha wa Brazil Dunga ameponda kulaumiwa kwa Kikosi cha Timu yake baada ya kutupwa nje toka kwenye Mashindano ya Copa America yanayoshindaniwa na Nchi za Marekani ya Kusini.
Brazil ilitupwa nje kwenye Robo Fainali ya Copa America na Paraguay baada kutoka Sare 1-1katika Dakika 90 na kushindwa kwa Mikwaju ya Penati 4-3 huku wakicheza bila ya Kepteni wao Neymar aliefungiwa baada ya Mechi ya PIli ya Kundi lao la Mashindano hayo baada ya kupewa Kadi Nyekundu kwenye Mechi na Colombia.
Dunga ameeleza: "Brazil ilikwenda Miaka 40 bila Copa America [1949 hadi 1989] na tulikuwa tukishinda kwingineko. Halafu tukaanza kushinda Copa America [Mataji 5 tangu 1989] na tukaambiwa Kombe hilo halina maana, muhimu ni Kombe la Dunia."
Aliongeza: "Tulipocheza Kombe la Mabara na kushinda, tukaambiwa halina maana. Sasa Vyombo vya Habari vimeamua Copa America ni muhimu. Soka ndio ilivyo!"
Akiwa kama Mchezaji, Dunga alitwaa Copa America mara 2 [1989 na 1997] na kisha kulibeba akiwa Kocha wa Brazil Miaka 8 iliyopita katika himaya yake ya kwanza kama Kocha .
Dunga alirudi tena kama Kocha wa Brazil Mwaka Jana baada ya Fainali za Kombe la Dunia na kuiongoza Brazil kushinda Mechi 11 na kufungwa Mechi 2 kwenye Copa America hii na kuamsha hisia mbaya toka Nchini kwao.
Brazil ndiyo Nchi inayoshikilia Rekodi ya kutwaa Kombe la Dunia mara nyingi baada ya kulibeba mara 5 ikifuatiwa na Italy na Germany zilizotwaa mara 4 kila mmoja, Argentina na Uruguaya mara 2 kila mmoja huku England, France na Spain zikitwaa mara 1 kila mmoja.

Hakuna maoni: