tecno

tecno

airtel

airtel

.

.

nido

nido

RADIO LISTEN NOW

30 Juni 2015

BARCA NA JUVE ZAKUTANA KUHUSU POGBA!

JUVE-POGBAKlabu za Barcelona na Juventus zilikutana Jana kujadili Uhamisho wa Staa anaechipukia kwa kasi Paul Pogba.
Vyanzo vya habari hizo, likiwemo La Gazzetta dello Sport la huko Italy, vimedai Mkurugenzi wa Juve, Beppe Marotta na Msimamizi stadi wa Uhamisho wa Barca, Ariedo Braida, walikutana Mjini Milan, Italy.
Ajenda ya Mkutano huo ilikuwa ni moja tu na nayo ni kujadili Uhamisho wa Pogba kutoka Juve kwenda Barca.
Suala la kumchukua Paul Pogba kwenda kuchezea Barca limekuwa moja ya Ilani za Uchaguzi wa Rais wa Barcelona ambao Rais wa sasa Josep Maria Bartomeu anachuana na Rais wa zamani Joan Laporta ambae yeye ameweka suala la kumnasa Pogba ndio silaha yake wakati wa Kampeni za Uchaguzi huo.
Hata hivyo La Gazzetta dello Sport limesema haijalishi nani atakuwa Rais wa Barca kwani wote Bartomeu na Laporta wanamtaka Kijana huyo anaechezea pia Timu ya Taifa ya Ufaransa.
Licha ya Manchester City kumtaka Pogba, Mchezaji wa zamani wa Timu ya Vijana ya Mahasimu wao Man United, Barcelona ndio wanaodhaniwa watamnasa kwani hilo ndio chaguo binafsi la Pogba.
Lakini pia manufaa kwa Juve kufanya biashara na Barca ni kuwa hata Pogba akiuzwa sasa itabidi abakie Juve kwa vile Barca wapo kwenye Kifungo cha kutonunua Wachezaji hadi 2016.
 

Hakuna maoni: