tecno

tecno

airtel

airtel

.

.

nido

nido

RADIO LISTEN NOW

30 Juni 2015

MAN UNITED: JONES ASAINI MPYA, WACHEZESHA KAMARI WAFUNGA OFISI KUHUSU SCHNEIDERLIN KUJIUNGA!

Phil Jones 2544878bMchezaji kiraka wa Manchester United Phil Jones Leo hii amesaini Mkataba mpya utakaomweka Old Trafford hadiB1A9D1D345D54AA28277B7629945E378 Juni 2019 wakati huko Mitaani Kampuni za Kuchezesha Kamari zimesimamisha kupokea Beti za Mchezaji wa Southampton Morgan Schneiderlin kama atajiunga na Man United au la.
MKATABA MPYA
Phil Jones, mwenye Miaka 23, amesaini Mkataba mpya na Man United ambao utambakiza Klabuni hapo hadi Juni 2019 pamoja na nyongeza ya Mwaka mmoja juu yake.
Jones alianza kuichezea Man United Mwaka 2011 na ameshacheza Mechi 128 na kutwaa Ubingwa wa Ligi Kuu England mara moja Mwaka 2013.
Akiongea baada ya kusainiwa Mkataba huo mpya, Meneja Louis van Gaal alisema: "Tumefurahi Phil amesaini Mkataba mpya. Yeye ni Mchezaji mwenye kipaji anaeweza kucheza nafasi nyingi. Bado ni  Kijana anae endelea wakati wote." 
Nae Phil Jones ameeleza: "Nimefurahishwa kusaini dili mpya. Hii ni Klabu kubwa kushiriki nayo na naungoja kwa hamu Msimu mpya."
BETI ZA SCHNEIDERLIN KUJIUNGA
Huku kukiwa na habari kuwa Kiungo wa Southampton Morgan Schneiderlin atajiunga na Manchester United Jumatano Julai 1 wakati Dirisha la Uhamisho litakapofunguliwa rasmi, Wachezesha Kamari wamesimamisha kupokea Beti za Mchezaji huyo kama atajiunga na Man United au la na hii ni dalili kubwa kuwa Uhamisho huo una uhakika.
Schneiderlin, Mchezaji wa Kimataifa wa France alieng'ara mno na Southampton katika Misimu Miwili iliyopita, amekuwa akiwindwa pia na Arsenal lakini inaelekea imebwaga manyanga.
Katika Siku za nyuma, Meneja wa Arsenal, Arsene Wenger, ashawahi kuulalamikia mkono wa Manchester United katika Uhamisho wa Wachezaji kwa kudai: "Kila Mchezaji anaeletwa kwangu, Manchester United wanakuwa tayari washafika!"
morgan
Imeripotiwa kuwa Man United na Southampton zimeshakubaliana Ada ya Uhamisho ya Pauni Milioni 25 kwa ajili ya Schneiderlin mwenye Miaka 25 ambae nae ashaafikiana kuhusu Maslahi yake binafsi ikiwemo kuzoa Mshahara wa zaidi ya Pauni 100,000 kwa Wiki.

Hakuna maoni: