MARADONA AMKARIBISHA CARLOS TEVEZ LA BOMBONERA!
Msimu uliopita, Tevez, mwenye Miaka 31 na ambae huitwa Apache huko
kwao, alipiga Bao 20 kwenye Ligi Serie A Msimu huu uliokwisha Majuzi na
kuisaidia Juventus kutwaa tena Ubingwa wa Italy.
Lakini Staa huyo wa Argentina hivi sasa anahusishwa kuihama Juve na
Klabu za Liverpool, Atletico Madrid na Paris St-Germain pia zinatajwa
kumlenga ingawa yeye mwenyewe ameshakaririwa mara kadhaa akisisitiza
mapenzi yake ya kurudi kule alikoanzia, La Bombonera, ambako alichezea
Timu ya Kwanza kuanzia 2001 hadi 2004.
Hivi sasa Tevez yuko Nchini Chile akiwa na Kikosi cha Argentina kinachoshiriki Copa America.
Maradona, ambae aliichezea Boca Juniors na kisha kuwa Makamu wa
Rais wake na pia Kocha wa Argentina kati ya 2008 na 2010 huku Tevez
akiwemo kwenye Kikosi hicho, ametumia ukurasa wake wa Mtandao wa
Facebook kumkaribisha tena Carlos Tevez Klabuni Boca Juniors.
Akiwa na Boca Juniors, Tevez alicheza Mechi 110 na kufunga Bao 38
na pia kutwaa Ubingwa Mwaka 2003 na vile vile kushinda Tuzo ya Mchezaji
Bora wa Marekani ya Kusini kwa Misimu Mitatu mfululizo.
Kabla Msimu wa 2005 kuanza, Tevez akahamia Klabu ya Brazil
Corinthians na Mwaka uliofuatia kujiunga na West Ham huko England kisha
kwenda Manchester United na Manchester City.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni