tecno

tecno

airtel

airtel

.

.

nido

nido

RADIO LISTEN NOW

21 Juni 2015

MARADONA AMKARIBISHA CARLOS TEVEZ LA BOMBONERA!

 83746779 tevezLenjendari wa Boca Juniors Diego Maradona amemkaribisha Carlos Tevez Klabuni hapo huku kukiwa na uvumi mkubwa kuwa Straika huyo wa Juventus yuko mbioni kurejea Klabu yake ya zamani maarufu kwa jina la La Bombonera.
Msimu uliopita, Tevez, mwenye Miaka 31 na ambae huitwa Apache huko kwao, alipiga Bao 20 kwenye Ligi Serie A Msimu huu uliokwisha Majuzi na kuisaidia Juventus kutwaa tena Ubingwa wa Italy.
Lakini Staa huyo wa Argentina hivi sasa anahusishwa kuihama Juve na Klabu za Liverpool, Atletico Madrid na Paris St-Germain pia zinatajwa kumlenga ingawa yeye mwenyewe ameshakaririwa mara kadhaa akisisitiza mapenzi yake ya kurudi kule alikoanzia, La Bombonera, ambako alichezea Timu ya Kwanza kuanzia 2001 hadi 2004.
Hivi sasa Tevez yuko Nchini Chile akiwa na Kikosi cha Argentina kinachoshiriki Copa America.
Maradona, ambae aliichezea Boca Juniors na kisha kuwa Makamu wa Rais wake na pia Kocha wa Argentina kati ya 2008 na 2010 huku Tevez akiwemo kwenye Kikosi hicho, ametumia ukurasa wake wa Mtandao wa Facebook kumkaribisha tena Carlos Tevez Klabuni Boca Juniors.
Akiwa na Boca Juniors, Tevez alicheza Mechi 110 na kufunga Bao 38 na pia kutwaa Ubingwa Mwaka 2003 na vile vile kushinda Tuzo ya Mchezaji Bora wa Marekani ya Kusini kwa Misimu Mitatu mfululizo.
Kabla Msimu wa 2005 kuanza, Tevez akahamia Klabu ya Brazil Corinthians na Mwaka uliofuatia kujiunga na West Ham huko England kisha kwenda Manchester United na Manchester City.

Hakuna maoni: