Mchezaji wa zamani wa Brazil ataka mikoba ya Blatter FIFA
Zico mwenye miaka 52 na ambaye
jina lake halisi ni Arthur Antunes Coimbra amesema, ni wajibu wake
kugombea. Akizungumza na kundi kubwa la waandishi wa habari katika kituo
chake cha kufundisha soka huko mjini Rio de Janerio, Zico amesema ni
huzuni kwenye michezo kuona kile kinachotokea katika soka leo hii. Kuona
rushwa, lakini pia kuona uchapakazi unaofanywa na baadhi ya watu wazuri
ukipotezwa. Pia aliongeza kuwa, ni wajibu wake sasa kutumia uzoefu na
ujuzi wake kujaribu kugombea nafasi ya urais.
Hivi karibuni rais wa shirikisho
hilo Sepp Blatter, alitangaza kuwa atajiuzuru wadhifa wake huo ikiwa ni
siku nne tu baada ya kuchaguliwa tena kushika madaraka hayo. Uamuzi huo
wa Blatter ulikuja ikiwa ni siku chache tu baada mamlaka ya Marekani na
Uswiz kufungua kesi ya rushwa kwa baadhi ya maafisa wa ngazi za juu
kwenye shirikisho la FIFA.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni