Higuain
amefunga goli pekee lililoipeleka Argentina kwenye hatua ya robo
fainali ya michuano ya Copa America inayozidi kushika kasi huko Chile.
Goli la Argentina limefungwa mapema kipindi cha kwanza dakika ya 11,
goli hilo liliipa Argentna ushindi wa goli 1-0 mbele ya Jamaica ‘Reggae
boys’ ambao hawajashinda mchezo wowote kwenye kundi B.
Ushindi huo unaifanya Argentina
kumaliza ikiwa kinara wa kundi B na huenda ikakutana na Ecuador, Peru au
Venezuela kwenye mtanange wa robo fainali utakaopigwa siku ya Ijumaa.
Nyota
wa Argentina na klabu ya Barcelona Lionel Messi alicheza mechi yake ya
100 akiwa ndani ya uzi wa Argentina akiisaidia timu yake kufuzu na
kusonga mbele kwenye hatua ya robo fainali. Messi ambaye mpaka sasa bado
hajatwaa taji lolote akiwa na timu yake ya taifa licha ya mafanikio
makubwa aliyopata kwenye ngazi ya klabu, mafanikio makubwa aliyopata
akiwa na timu ya taifa ni kuifikisha timu hiyo kwenye fainali ya kombe
la dunia mwaka jana dhidi ya Ujerumani lakini timu yake iliambulia
kichapo na kombe hilo likaenda Ujerumani.
Mchezo
wa kwanza wa kundi B uliikutanisha Uruguay dhidi ya Paraguay ambapo
pambano hilo lilimalizika kwa timu hizo kwenda sare ya kufungana goli
1-1 lakini Uruguay wamekata tiketi ya kucheza robo fainali ya michuano
hiyo.
Jose Gimenez alianza kuifungia
Uruguay goli la kuongoza dakika ya 29 ya mchezo lakini Lucas Barrios
aliisawazishia Paraguay goli hilo japo sare hiyo haijawasaidia Paraguay
kusonga mbele kwenye mashindano hayo makubwa kwa bara la Amerika ya
Kusini.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni