tecno

tecno

airtel

airtel

.

.

nido

nido

RADIO LISTEN NOW

21 Juni 2015

THIERRY HENRY-ALEXIS SANCHEZ ATAIPA UBINGWA ARSENAL... WAKIONGEZA WAPYA!!!!!!!

Arsene-Wenger-UchunguHuku wakiripotiwa kukaribia kumnasa Kipa wa Chelsea Petr Cech, Lejendari wa Arsenal, Thierry Henry, amedai ikiwa Meneja Arsene Wenger ataimarisha Kikosi basi Winga wao kutoka Chile, Alexis Sanchez, atawapa Ubingwa wa England ambao mara ya mwisho kuutwaa ni Miaka 11 iliyopita.
Wachezaji wanaohusishwa na kutua Arsenal ni pamoja na Fowadi wa FC Porto, Jackson Martinez, Kiungo wa AS Monaco Geoffrey Kondogbia, Mchezaji wa  Borussia Dortmund Sven Bender na Kiungo toka Southampton, Morgan Schneiderlin.
Akiongelea kuhusu hali ya Arsenal, Thierry Henry, ambae ndie anashikilia Rekodi ya Ufungaji Bora ya Arsenal na alikuwa Mchezaji wa kile Kikosi cha Timu hiyo cha 2003/04 ambacho hakikufungwa kwenye Ligi Msimu mzima, amesema: "Kama shabiki wa Arsenal, naungoja kwa hamu Msimu ujao na natarajia tutaleta wapya, Wachezaji wapya lakini kama unae mtu kama Alexis Sanchez, lolote linaweza kutokea. Anaweza kutupa Ubingwa!"
Aliongeza: "Tizama alivyofanya kwenye Fainali ya FA CUP na nini amekuwa akifanya tangu aje hapa. Amekuwa ni hatari! "
Katika Msimu wake wa kwanza na Arsenal, Sanchez alifunga Bao 24.

Hakuna maoni: