PETR CECH AIKARIBIA EMIRATES!
Kipa wa Chelsea Petr Cech anakaribia kuhamia Arsenal kwa m
Cech, mwenye Miaka 33, ameshaafikiana maslahi yake binafsi na
Arsenal na kilichobaki ni kusawazisha mvutano kati ya Chelsea na Arsenal
kuhusu Ada ya Uhamisho huku pande hizo mbili zikikubaliana kuendelea na
mazungumzo.
Cech amebakiza Mwaka mmoja katika Mkataba wake na Chelsea na
ameruhusiwa rasmi na Mmiliki wa Klabu hiyo, Roman Abramovich, kuhamia
Klabu yeyote anayotaka baada ya kusugua Benchi Msimu uliopita akiwa Kipa
Namba mbili nyuma ya Thibaut Courtois.
Cech alijiunga na Chelsea Mwaka 2004 akitokea Klabu ya France Rennes na kuidakia Chelsea Mechi 333.
Ingawa Cech mwenyewe anapendelea kubakia London na hivyo kujiunga
na Arsenal, Meneja wa Chelsea Jose Mourinho hataki hilo na alipendelea
Kipa huyo wa Kimataifa kutoka Czech Republic ahamie kwa Mabingwa wa
France Paris Saint-Germain.
Lakini Karata ya Trufu ya Mmiliki Roman Abramovich ndiyo imemtoa kapa Jose Mourinho na kumpa mtaji Kipa Mkongwe Petr Cech.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni