tecno

tecno

airtel

airtel

.

.

nido

nido

RADIO LISTEN NOW

11 Juni 2015

Sio bure: Daktari afichua siri ya mafanikio ya Lionel Messi

messi-2011_3303486b
Nyota wa klabu ya soka ya Barcelona,  Muargentina Lionel Messi aliachana na vyakula vya kisasa vya dukani ‘super market’ na kuamua kutumia vyakula vya asili.
Daktari wa mchezaji huyo bora mara nne wa dunia, Giuliano Poser amethibitisha kuwa ilibidi kufanya mabadiliko ya chakula ili kumrudisha kwenye fomu yake ya zamani mchezaji huyo.
Itakumbukwa kuwa Lionel Messi alipoteza mara mbili mfululizo tuzo ya uchezaji bora wa dunia,  Ballon D’or kwa mpinzani wake wa muda mrefu Cristiano Ronaldo baada ya kutokuwa na uwezo wake mzuri wa awali.
Pamoja na klabu yake ya Barcelona kutofanya vizuri ndani ya misimu hiyo miwili mfululizo, pia Messi alishindwa kuisaidia timu yake ya taifa ya Argentina ilipofungwa 1-0 dhidi ya mabingwa wa sasa wa dunia Ujerumani kwenye mechi ya fainali ya kombe la dunia la FIFA nchini Brazil mwaka jana.
Inaelezwa kuwa baada ya kuanza vibaya msimu huu uliomalizika kwa Barcelona kushinda vikombe vyote vitatu walivyoshiriki ‘treble’ Lionel Messi alimtafuta daktari huyo Giuliano Poser ambaye aliwahi kumsadia mwaka 2008 alipokuwa na matatizo ya kiafya.
Poser anasema, “mara baada ya kombe la dunia, kila kitu kilibadilika kwa Messi” amezungumza daktari huyo wakati akiongea na gazeti la Delo Sport la Hispania.
“Messi ni kijana mpole na mtulivu. Hakuwa vizuri na akahisi kuna kitu kinahitaji mabadiliko” Poser anaeleza
Barcelona walianza kwa kususua msimu huu na hata kupelekea mikwaruzano baina ya wachezaji na kocha wao Jose Enrique, lakini mambo yalibadilika ghafla na kushuhudia wakirudi katika mstari na fomu ya Messi ikawa ndio chachu ya wao kumaliza na vikombe vyote walivyoshiriki msimu huu.
“Alibadilisha chakula, hatumii tena vyakula vya dukani. Anakula vyakula vyenye utajiri wa vitamin, madini, mbogamboga na maziwa.” Anamalizia Poser daktari wa mchezaji huyo.

Hakuna maoni: