tecno

tecno

airtel

airtel

.

.

nido

nido

RADIO LISTEN NOW

21 Julai 2015

'MESSI NI PELE WA KIZAZI HIKI!'

MESSI-COPABEKI wa zamani wa Barcelona na Chelsea, Juliano Belletti, amemsifia Lionel Messi na kumtaja kuwa ndie 'Pele wa Kizazi hiki.'
Pele, Lejendari wa Brazil ambae Jina lake kamili ni Edson Arantes do Nascimento, ndie anaesifika kuwa  Mchezaji Bora kabisa katika Historia ya Soka kwa kuiwezesha Brazil kutwaa Kombe la Dunia maraa 3.
Messi, mwenye Miaka 28, alififia mwanzoni mwa Msimu uliopita lakini akalipuka baadae na kuibeba Barcelona kutwaa Trebo, yaani Ubingwa wa La Liga, Copa del Rey na UEFA CHAMPIONZ LIGI.
Hata hivyo, Messi amepondwa Nchini kwao Argentina baada ya kushindwa kutwaa Copa America walipobwagwa na Chile kwenye Fainali.
pele
Belletti, Raia wa Brazil ambae alitwaa Ubingwa wa La Ligas mara 2 na UEFA CHAMPIONZ LIGI mara moja akicheza na Messi huko Barcelona, anaamini Messi hana mfano katika kizazi hiki na hastahili kuzomewa huko kwao Argentina.
"Messi ndio Pele wa kizazi hiki," Amenena Belleti, "Sielewi kwanini kwao wanamponda. Huwezi kumponda Mchezaji kama Messi. Lakini hii pia ilitokea kwa Ronaldinho huko Brazil. "
Belletti pia alimtetea Mbrazil mwenzake Neymar ambae alitolewa kwa Kadi Nyekundu kwenye Copa America na kisha kufungiwa Mechi 4 na kuzikosa Mechi za Brazil ambayo ilikuja kutolewa Robo Fainali.
Kuhusu Neymar, Belletti amesema: "Bado ni Kijana. Watu wanadhani ana Umri mkubwa. Bado ana muda wa kukomaa."

Hakuna maoni: