HIZI NDIO DHAHABU ZA MSIMU ULIOPITA ZILIZOGEUKA MAKAA YA MAWE MSIMU HUU…
Nikiwa nimekaa kwenye kiti changu
cha mbao maarufu kama ‘benchi’ nilishangaa sana kuona umati wa watu
ukishangilia goli la kichwa cha kufunika cha Andrew Ayew, binafsi
sikushangilia kwani bado nilikuwa nasikia harufu ya damu.
Japokuwa Montero hakuwepo ila
bado niliamini lazima shetani achinjwe tena kifo kibaya hasa kutokana na
uwepo wa Bafetimbi Gomis pale mbele. Kabla sijaisoma ‘sms’ iliyoingia
kwenye simu yangu niliona pasi ya Ayew inamfikia Gomis
katikati ya mabeki wawili wa Van Gaal, kwakweli hadi sasa sijui
kiliendelea nini….
Anyway tuachane na huo unafiki wa
kisoka maana ndio raha yenyewe ya mchezo huu unaopendwa sana hapa
duniani pengine kuliko michezo yote. Soka ni mchezo wa ajabu sana kwani
maajabu pia yana nafasi yake katika tasnia hii. Msimu uliopita kuna
baadhi ya timu zilianza vyema sana ila msimu huu mambo yamebadilika sana
hadi watu wanashika vichwa. Hapa chini nimekuweeka timu ambazo zilianza
vyema ila msimu huu mabo
magumu kama chaguzi za wanachama wa TFF huko mikoani, karibu sana…
magumu kama chaguzi za wanachama wa TFF huko mikoani, karibu sana…
BORUSSIA MONCHENGLADBACH
Msimu uliopita Borussia Monchengladbach walishika nafasi ya tatu huku wakitoa changamoto kibao licha ya kutolewa mapema kwenye michuano ya Europe League. Usajili waliofanya inawezekana uliwapa kitu cha ziada
jamaa hawa ambao wapo kundi moja na Man City. Katika mechi tatu za mwanzo msimu 2014/15, Monchengladbach hawakufungwa mechi hata moja licha ya kuanza kwa sare mbili dhidi ya VfB Stuttgart na SC Feiburg kabla ya kuirarua Schalke 04 mabao 4-1 na kukamilisha pointi tano kwenye mechi tatu.
Msimu uliopita Borussia Monchengladbach walishika nafasi ya tatu huku wakitoa changamoto kibao licha ya kutolewa mapema kwenye michuano ya Europe League. Usajili waliofanya inawezekana uliwapa kitu cha ziada
jamaa hawa ambao wapo kundi moja na Man City. Katika mechi tatu za mwanzo msimu 2014/15, Monchengladbach hawakufungwa mechi hata moja licha ya kuanza kwa sare mbili dhidi ya VfB Stuttgart na SC Feiburg kabla ya kuirarua Schalke 04 mabao 4-1 na kukamilisha pointi tano kwenye mechi tatu.
Msimu huu timu hii imeanza vibaya
sana kwani katika mechi tatu hadi sasa haijapata ushindi wala sare
yeyote. Monchengladbach ndiyo timu inayoshikilia mkia katika mechi tatu
za Bundesliga hadi sasa.
Walianza kwa
kipigo cha 4-0 kutoka kwa Dortmund, kichapo cha 2-1 nyumbani kutoka kwa
Mainz 05 kabla ya kulala 2-1 juzi kutoka kwa Weder Bremen. Tayari
imeruhusu magoli nane hadi sasa bila pointi yoyote. Japokuwa bado ni mapema ila wanapaswa kujipanga upya mapema.
JUVENTUS
Msimu uliopita timu ya Juventus ilianza kwa kasi kama ilivyofanya pia misimu ya nyuma kabla ya msimu huo. Utakumbuka Juventus walimaliza ligi kwa kukusanya pointi 87 huku pia wakifanya vizuri kwenye ligi ya mabingwa barani Ulaya.
Msimu uliopita timu ya Juventus ilianza kwa kasi kama ilivyofanya pia misimu ya nyuma kabla ya msimu huo. Utakumbuka Juventus walimaliza ligi kwa kukusanya pointi 87 huku pia wakifanya vizuri kwenye ligi ya mabingwa barani Ulaya.
Juve walishinda mechi zao tatu za
mwanzo kwani walianza kwa ushindi wa 1-0 ugenini dhidi ya Chievo kabla
ya kuirarua Udinesse 2-0 na kuwamaliza kabisa Milan 1-0 pale Sansiro.
Matokeo haya yalidhihirisha beki bora ya Juventus kwa kutoruhusu goli
ndani ya mechi hizi.
Msimu huu, Juventus wameanza
vibaya sana tena zaidi ya sana. Kipigo cha mabao 2-1 kutoka kwa AS Roma
kilikuwa ni mwendelezo wa kile cha 1-0 kutoka kwa Udinese nyumbani. Hali
hii inawafanya mabingwa hawa wa Italia kukamilisha mechi hizi bila pointi yoyote kitu ambacho sio kawaida.
Mechi ijayo wanacheza na Chievo
Verona nyumbani, Massimiliano Allegri anasubiriwa kwa hamu kuona kama
ataweza kuchukua pointi tatu kwa mara ya kwanza ndani ya msimu huu.
OLYMPIC MARSEILLE
Olympic Marseille ni timu nyingine ambayo vyombo vingi vya habari haviangalii mwenendo wake wa msimu uliopita na msimu huu inawezekana ni kwa sababu ya kutekwa na Uingereza na Uhispania. Msimu uliopita timu hii ilishika nafasi ya nne kwa kuwa na pointi 69.
Olympic Marseille ni timu nyingine ambayo vyombo vingi vya habari haviangalii mwenendo wake wa msimu uliopita na msimu huu inawezekana ni kwa sababu ya kutekwa na Uingereza na Uhispania. Msimu uliopita timu hii ilishika nafasi ya nne kwa kuwa na pointi 69.
Katika mechi zake nne za mwanzo,
Marseille ilikusanya pointi sba kati ya 12. Marseille ilitoa vipigo kwa
Guingamp na Nice baada ya kutoa sare na Bastia kabla ya kipigo cha 2-0
kutoka kwa Montpellie. Pointi saba zilikuwa muhimu sana kwao.
Msimu huu watu walidhani kwamba timu hii itarejesha makali
yake lakini imekuwa ndivyo sivyo japokuwa ni mapema sana kuwahukumu
ndani ya mechi nne za French League 1. Ndani ya mechi hizi timu hii
imekusanya pointi tatu pekee huku ikipoteza mechi tatu kwa kupigwa na
Caen, Reims na Guingamp. Japokuwa walishinda magoli sita kwa Troyes
mechi iliyopita kabla ya jana ila bado jana walipokea kipigo ugenini.
Mwanzo huu bado sio mzuri kwa timu hii inayonolewa na Marcelo Bielsa.
CHELSEA FC
Timu hii ilianza kwa kasi sana msimu uliopita kwa kutoa dozi kwa kila aliyekutana nae muda wowote. Utakumbuka Chelsea ya mwaka jana ilikuwa inapewa nafasi ya kumaliza ligi bila kupoteza mechi kabla ya
kusimamishwa na Newcastle kwa mara ya kwanza. Blues walikusanya pointi 12 kwenye mechi nne za mwanzo dhidi ya Burnley, Leicester, Everton na Swansea huku ikiruhusu magoli sita na kufunga magoli 15 ya haja. Matokeo haya yalifanya wachambuzi waipe nafasi tena Chelsea msimu huu.
Timu hii ilianza kwa kasi sana msimu uliopita kwa kutoa dozi kwa kila aliyekutana nae muda wowote. Utakumbuka Chelsea ya mwaka jana ilikuwa inapewa nafasi ya kumaliza ligi bila kupoteza mechi kabla ya
kusimamishwa na Newcastle kwa mara ya kwanza. Blues walikusanya pointi 12 kwenye mechi nne za mwanzo dhidi ya Burnley, Leicester, Everton na Swansea huku ikiruhusu magoli sita na kufunga magoli 15 ya haja. Matokeo haya yalifanya wachambuzi waipe nafasi tena Chelsea msimu huu.
Msimu wa sasa mambo ni magumu kwa
vijana hawa wa Mourinho kwani wamefanya madudu ya kutosha baada ya
kuruhussu magoli tisa ndani ya mechi nne huku wakifunga magoli sita
pekee. Hadi sasa Chelsea ina pointi nne kati ya 12 walizopaswa
kukusanya. Chelsea imeshinda mechi moja pekee tena
kibahati kwani walikuwa wanaomba mpira uishe. Jose Mourinho anapaswa kuchanga karata zake vyema kwani ana mechi ngumu zinazomkabili na asipoangalia ataanza kunyooshewa vidole na Abromovich.
kibahati kwani walikuwa wanaomba mpira uishe. Jose Mourinho anapaswa kuchanga karata zake vyema kwani ana mechi ngumu zinazomkabili na asipoangalia ataanza kunyooshewa vidole na Abromovich.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni