tecno

tecno

airtel

airtel

.

.

nido

nido

RADIO LISTEN NOW

3 Septemba 2015

BAADA YA KUKATALIWA KUUZWA, BERAHINO AKATAA KUICHEZEA TENA WBA

BerahinoMshambuliaji mwingereza mwenye asili ya Burundi Saido Berahino amejikuta katika ugomvi mkubwa na mwenyekiti wa klabu yake ya West Bromwich Albion na ndugu Jeremy Peace baada ya kugomewa kuuzwa na kuahidi kutochezea tena klabu hiyo.
Klabu ya Tottenham Hotspur ya London ilikataliwa ofa zake tatu za kutaka kumsajili mshambuliaji huyo mwenye miaka 22 ili amsaidie Harry Kane katika safu ya ushambuliaji ya klabu hiyo.
Spurs walipeleka mara ya mwisho dau la pauni 25m kwa kijana huyo mzaliwa wa Burundi aliyehamia Uingereza na wazazi wake kutokana na vita ya Burundi, lakini mwenyekiti wa West Bromwich bwana Jeremy Peace alikataa kata kata kumuachia mchezaji huyo.
Kuelekea kufungwa kwa dirisha la usajili usiku wa tarehe 1 September, Saido Berahino kupitia ukurasa wake wa Twitter aliandika kwa hasira kwamba anashindwa kutafuta maneno ya kuelezea hisia zake, lakini akasema kamwe hatoichezea tena timu ya Jeremy Peace akimaanisha West Bromwich.
Kwa takribani wiki tatu hivi sasa, Saido Berahino hakua katika hali nzuri kiakili kutokana na kutaka kuichezea klabu ya Tottenham Hotspur iliyokuwa ikimhitaji kwa udi na uvumba, kitu kilichopelekea kocha wake Tony Pulis asimchezeshe katika mechi zote tatu ilizocheza timu yake.
Tayari Tony Pulis ameeleza kusikitishwa kwake na hali tete iliyopo kati ya Berahino na mwenyekiti wake huku akisisitiza itakua kazi ngumu zaidi kurudisha mahusiano ya Berahino na klabu kwa haraka.
Pulis amejitetea kwamba Tottenham Hotspur walichelewa kuleta ofa nzuri na kwamba wao kama West Bromwich wangeshindwa kupata mfungaji mwingine wa magoli na ndicho kilichopelekea wao kutokuwa tayari kumuachia kijana huyo anaezungumza kiswahili vizuri.

Hakuna maoni: