MADINI ADIMU USIYOYAJUA KUTOKA KWA BEKI MPYA WA CHELSEA PAPY DJILOBODJI
Na Salym Juma
Mimi sio miongoni mwa mashabiki
wa Chelsea na sina timu kabisa Uingereza, kila siku nawaambia timu yangu
ni ‘BvB’ naamini wale wazee wa Bundesliga mnaifahamu timu hii. Japokuwa
sina timu ila kuna vitu vinanifurahisha pale na vingine vinanihuzunisha
sana pale EPL. Bafetimbi Gomiz na Wayne Rooney wananifurahisha sana
kutokana na viwango vyao! Najua kuna watu nawagusa hapa ila ‘CYBER
CRIME’
inanilinda. Ivanovic na Pedro
wananipa raha sana kutokana na viwango yao matata…! Najua kuna watu
wamekunja uso hapa, Anyway mtajua wenyewe ila ‘Unafiki’ siachi ng’oo…….
“Ni mara chache sana nimekutana na beki anayetumia miguu yote na anacheza vizuri kwa kutumia miguu hii” Yaya Toure.
Kama wewe ni mpenzi mzuri wa
mipira ya Kia-afrika utakuwa unafahamu kauli hii ya mchezaji huyu
aliitoa wapi na lini. Kutokana na mapungufu yaliyopo kwenye idara ya
ulinzi ya Chelsea, hivi karibuni Jose
Mourinho alinasa saini ya mchezaji mkubwa mwenye jina dogo, anayecheza ligi ndogo na timu isiyojulikana kabisa kwa watu walioujua mpira karibuni. Naamini wengi mnafahamu mchezaji wa Kisenegali ndiye anayezungumziwa hapa na sio mwingine bali ni Papis Mison Djilobodji, kijana mwenye miaka 26 aliyetua kuimarisha idara ya ulinzi ya Chelsea.
Mourinho alinasa saini ya mchezaji mkubwa mwenye jina dogo, anayecheza ligi ndogo na timu isiyojulikana kabisa kwa watu walioujua mpira karibuni. Naamini wengi mnafahamu mchezaji wa Kisenegali ndiye anayezungumziwa hapa na sio mwingine bali ni Papis Mison Djilobodji, kijana mwenye miaka 26 aliyetua kuimarisha idara ya ulinzi ya Chelsea.
Kutokana na usaili huu
kuzungumzwa sana mitaa mbalimbali ya nchi hii ambayo anatokea msanii
mkubwa Afrika anayeitwa Diamond Platnum, leo hii nimekuletea vitu adimu
ambavyo pengine huvijui kutoka kwa mchezaji huyu aliyecheza mechi 13
kwenye timu yake ya taifa. Karibu sana…
BEKI MKAKAMAVU NA MGUMU PALE NYUMA
Unapozungumzia mabeki hodari
kwenye ligi kuu ya Ufaransa huwezi kumuacha mlinzi huyu japokuwa
hakutajwa sana kutokana na majina ya akina David Luis na Thiago Silva
kuwa maarufu kwenye vinywa vya wanasoka wengi hasa wale walioanza
kufuatilia mpira miaka ya hivi karibuni. Papy Djilobodji (26) ni beki
mzuri sana anayehitajika na kocha makini kama Jose Mourinho ila
kinachomgharimu ni umri pekee kwani Mou alihitaji beki mwenye chini ya
miaka 23 ili aweze kutengeneza ‘Partnership’ na akina Kourt Zouma, Baba
Rahman na Cesar Azipilicueta.
Papy kama beki makini ana wastani
wa kufanya ‘Clearance’ 8.3 kwa mechi moja, pia amefanya ‘Interception’
3.3 kwa mechi moja na huu ni wastani mzuri sana. Pia kafanya jumla ya
‘Interception’ 101 na kumfanya kuwa juu katika kipengele hiki kuliko
beki yoyote wa Chelsea. Papy pia akiwa kama Mlinzi pale nyuma, licha ya
timu yake kumaliza nafasi ya 14, waliruhusu magoli 40 ndani ya mechi 38
za ligi. Sasa itakuaje kama atacheza sambamba na mabeki wa kiwango cha
dunia pale nyuma? Kwa takwimu hizi ni wazi tusubiri makubwa kutoka
kwake.
ANATUMIA MIGUU YOTE, MREFU NA MWEPESI SANA
Msenegali huyu ana faida tatu
tajwa hapo juu. Nguvu pia ni faida nyingine ambayo kijana huyu anayo na
hatimaye kuwa tofauti na wachezaji wengine. Urefu wake ni futi 6 na
inchi 4, kutokana na hili jamaa ana wastani mzuri sana wa kupiga mipira
ya juu hasa ile ya vichwa pindi inapokuwa langoni mwake na kwenye goli
la wapinzani pia. Papy ana wastani wa kuokoa mipira ya vichwa kwa 3.1
katika mechi moja. Pia jamaa anatumia miguu yote na hivo anaweza kucheza
nafasi zote kama Mdogo wangu Cesar Azipilicueta. Wepesi wake utamfanya
afanye makubwa sana pale Darajani.
NI MCHEZAJI HODARI ANAYEWEZA KUCHEZA NAFASI TOFAUTI
Kama nilivyotanguia kukuambia
hapo kabla kuwa huyu jamaa anatumia miguu yote miwili, hivyo anaweza
kucheza nafasi zote kati ya zile 4 za pale nyuma. Papy pia anaweza
kucheza kama ‘Defensive-midfielder’ na wakati mwingine pia anaweza
kucheza kama ‘Holding-midfielder’ Kama wewe ni mfuatiliaji wa mbinu za
Jose Mourinho utakubaliana na mimi kuwa Mou anapenda wachezaji wanaoweza
kubadili nafasi Zaidi ya moja uwanjani kama akina Ramos, David Luiz,
Pepe na wachezaji wenye kaliba ya akina Nemanja Matic.
NI MFUNGAJI MZURI PALE ANAPOPATA NAFASI
Kutokana na urefu, wepesi na
ujanja wa Mchezaji huyu ni wazi kuwa analijua goli hasa kutokana na
takwimu zake za kufunga magoli tisa ndani ya mechi 171 kwenye Klabu
yake ya Nantes. Magoli haya ni mengi mno
kwani kuna mabeki kibao pale Chelsea na timu zingine wamecheza mechi kibao bila kuwa na magoli kama haya. Papy ni mzuri sana kwenye mipira ya kona na ile ‘Free kick’ kwani anafahamu goli lilipo na ni mzuri pia ‘Kuji-position’ wakati mipira hii inapigwa. Inawezekana akafanya makubwa sana endapo ataaminiwa na Mou kwani ni mchezaji mzuri mno.
kwani kuna mabeki kibao pale Chelsea na timu zingine wamecheza mechi kibao bila kuwa na magoli kama haya. Papy ni mzuri sana kwenye mipira ya kona na ile ‘Free kick’ kwani anafahamu goli lilipo na ni mzuri pia ‘Kuji-position’ wakati mipira hii inapigwa. Inawezekana akafanya makubwa sana endapo ataaminiwa na Mou kwani ni mchezaji mzuri mno.
KACHELEWA SANA KUPANDA NDEGE
Ndege ninayoizungumzia hapa ni
ile ya kuvuka bahari kwenda barani Ulaya. Papy kwa mara ya kwanza
alikwenda Ulaya akiwa na miaka 19 hasa baada ya kuonekana ni mchezaji
mzuri ila kama ilivyo kawaida, changaomoto katika maisha in kitu cha
lazima kwani Papy licha ya kiwango chake alifeli majaribio kwenye Vilabu
vya Lazio na Lile na hatimaye kuangukia kwenye timu ndogo ya Senart
Moissy iliyokuwa daraja la nne pale Ufaransa. Hali hii haikumkatisha
tamaa kwani alichez kwa bidii na kufikia hatua ya kusajili ligi kuu ya
Ufaransa na sasa ni anakwenda Chelsea.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni