tecno

tecno

airtel

airtel

.

.

nido

nido

RADIO LISTEN NOW

3 Septemba 2015

CHICHARITO AMPOTEZEA VAN GAAL, AAGA MASHABIKI, AMKUMBUKA FERGUSON

Javier Hernandez 'Chicharito' kushoto akiwa katinga uzi wa klabu yake mpya (kulia) ni mgurugenzi wa michezo wa Bayer Leverkusen Rudi Voller
Javier Hernandez ‘Chicharito’ kushoto akiwa katinga uzi wa klabu yake mpya (kulia) ni mgurugenzi wa michezo wa Bayer Leverkusen Rudi Voller
Mshambuliaji raia wa Mexico, Javier Hernandez ‘Chicharito’ ametoa salamu zake za mwisho za kuaga Manchester United huku akiwashukuru kocha Sir Alex Ferguson, mkuu wa maskauti Jim Lawlor pamoja na mashabiki, huku akiwapotezea kocha wa sasa wa Manchester United, Louis Van Gaal pamoja na aliyekua mrithi wa Ferguson, David Moyes.
Kupitia katika kurasa zake za mitandao ya kijamii Hernandez ambae alisajiliwa kujiunga na Manchester United mwaka 2010 akitokea Guadajala ya nyumbani kwao Mexico, amemshukuru kwa nafasi ya pekee mkuu wa maskauti wa Manchester United ndugu Jim Lawlor kwa kumsaidia kujulikana na dunia.
Aidha amempa sifa zake kocha legendari wa Manchester United, mstaafu Alex Ferguson kwa kumkuza kama mwanae huku akisema pia hatowasahau mashabiki wa Manchester United.
Hernandez hivi sasa amejiunga na klabu ya soka ya Bayern Leverkusen na kusisitiza amefurahi kuwa sehemu ambapo anaonekana ni mtu muhimu. Chicharito ambaye tangu kustaafu kwa kocha Alex Ferguson, alikua katika wakati mgumu kwenye klabu ya Manchester United chini ya walimu David Moyes na Louis Van Gaal.

Hakuna maoni: