tecno

tecno

airtel

airtel

.

.

nido

nido

RADIO LISTEN NOW

15 Septemba 2015

WACHEZAJI WA CHELSEA WAINGIWA NA HOFU

Chelsea hoiHofu imezidi kutanda miongoni mwa mastaa pamoja na benchi la ufundi la Chelsea kutokana na kuanza vibaya msimu huku wakionesha wasiwasi wao juu ya kuziba pengo la points baina yao na kiongozi wa ligi Manchester City.
Chelsea tayari imekwisha poteza michezo mitatu katika mechi tano za awali huku ikielezwa kuwa hali ya wasiwasi miongoni mwa wachezaji ikiwa ni kubwa zaidi.
Kocha Jose Mourinho hataki kupaniki na wala hajaitisha mkutano wowote wa ‘crisis’ kuelekea katika mchezo wa klabu bingwa Ulaya dhidi ya Maccabi Tel Aviv katika uwanja wa Stamford Bridge.
Chelsea imevuna points nne pekee katika katika michezo mitano ya ligi msimu huu, ikizidiwa points 11 na viongozi wa ligi Manchester City wenye points 15, kitu kinachowapa hofu wachezaji wa Chelsea namna gani ni vigumu kuziba pengo hilo.
Inaelezwa kuwa hali ya morali ya timu iko chini sana katika kikosi hicho, huku ukiwa ni mwanzo mbaya zaidi katika historia ya klabu tangu mwaka 1988.

Hakuna maoni: