tecno

tecno

airtel

airtel

.

.

nido

nido

RADIO LISTEN NOW

15 Septemba 2015

MKONGWE WA ARSENAL ATAJA MBADALA WA WENGER

Arsenal logo
Baada ya mashabiki wa Arsenal kulalamika sana kuhusu kocha wao na watu mbalimbali bado wanajaribu kutoa maoni yao nani anaweza kuwa kocha mpya.Robert Pires ametoa maoni yake juu ya nani anadhani angeweza kutwaa mikoba ya Arsene Wenger, na kusema kuwa ama Carlo Ancelotti au Thierry Henry ndio wanastahili kiti hicho japokuwa asingependa kuona Mfaransa huyo anaondoka hivi karibuni.
Wenger amekuwa katika msukumo mkubwa katika miezi ya hivi karibuni kutoka mashabiki wa Arsenal, ambao wanataka mafanikio ya haraka kwa timu yao, lakini Pires alipoulizwa alijibu, “Nani ni mbadala sahihi? Thierry Henry? ndio, analijua soka vizuri pamoja na Arsenal. Sijui…lakini nampenda zaidi Carlo Ancelotti”.
Wachezaji wa zamani wa kikosi cha Arsenal Robert Pires (kulia) na Thiery Henry (kushoto)
Wachezaji wa zamani wa kikosi cha Arsenal Robert Pires (kulia) na Thiery Henry (kushoto)
Lakini hata hivyo, Pires amegoma kusema kuwa kocha wake huyo wa zamani wakati wake umekwisha, kwa haraka alijibu hivi, “Lakini hayo ni maoni yangu tu, haina maana kwamba Arsenal inamhitaji Ancelotti kwa wakati huu. Wenger bado ana mkataba na Arsenal”.
Katika sehemu ambayo Wenger amekuwa akilaumiwa sana ni suala la usajili ili kukiboresha kikosi chake.
Lakini Pires analichukulia suala hilo kwa utofauti kidogo, na kusema, “Nisingependa kusema kuwa Arsenal wamefanya kosa lolote katika suala la usajili. Kama unaichezea Arsenal, maana yake ni kwamba una ubora fulani. Miongoni mwao ni wachezaji wakubwa sana ulimwenguni.
“Kwa upande wangu, usajili bora kabisa wa Arsenal ni Santi Cazorla. Mashabiki wanampenda Alexis Sanchez, je, vipi kwa upande wangu; Amekuwa ni mwepesi wa kuendana na mazingira ya ligi mpya ya EPL-lakini Cazorla ni mtu muhimu sana. Kwa miezi michache iliyopita , amekuwa ni mchezaji wetu bora”

Hakuna maoni: