tecno

tecno

airtel

airtel

.

.

nido

nido

RADIO LISTEN NOW

24 Januari 2016

ARSENAL ‘TEJA’ KWA CHELSEA, YATWANGWA KWAO EMIRATES, DIEGO COST ‘KILA!’

LIGI KUU ENGLAND
Matokeo:
Jumapili 24 Januari 2016
Everton 1 Swansea 2        
Arsenal 0 Chelsea 1
++++++++++++++++++++
CHELSEA-COSTA-AWALIZA-ARSENALKAMA kawaida yake, Diego Costa, ameacha gumzo kubwa baada ya kusababisha Sentahafu wa Arsenal apewe Kadi Nyekundu katika Dakika ya 18 na yeye kuifungia Chelsea Bao pekee BPL-JAN24Ana la ushindi katika Dakika ya 23.
Kipigo hiki cha 1-0 cha Chelsea kwa Arsenal ni muendelezo wa vipigo mfululizo kuanzia 2010 lakini Leo ndio cha kuuma sana kwani kimewatupa Arsenal Nafasi ya 3 kwenye Ligi Kuu England wakiwa nyuma ya Vinara Leicester City na Man City.
Arsenal, wakiwa kwao Emirates, walipata balaa Dakika ya 18 tu baada ya Sentahafu wao, Per Mertesacker, kumwangusha Diego Costa aliekuwa akichanja mbuga kumuona Kipa na Refa Mark Clattenburg kuamua ni Kadi Nyekundu ingawa tukio hili limegawa pande kila Mtu akibaki na nini alichoona yeye.
Upungufu huo ulimfanya Meneja wa Arsenal, Arsene Wenger, amtoe Straika Olivier Giroud, na kumwingiza Sentahafu Mbrazil Gabriel Paulista ambae ndie alitoa uchochoro Dakika 5 baadae kwa Diego Costa kufunga Bao pekee na la ushindi.
VIKOSI:
Arsenal: Cech; Bellerín, Koscielny, Mertesacker, Monreal; Flamini, Ramsey; Campbell, Özil, Walcott; Giroud
Akiba: Ospina, Chambers, Gibbs, Gabriel, Elneny, Oxlade-Chamberlain, Sánchez.
Chelsea: Courtois; Ivanovic, Zouma, Terry, Azpilicueta; Mikel, Matic; Willian, Fàbregas, Oscar; Costa
Akiba: Begovic, Cahill, Baba Rahman, Loftus-Cheek, Traore, Hazard, Rémy.
REFA: Mark Clattenburg
ARSENAL-CHELSEA-REDCARD
LIGI KUU ENGLAND
Ratiba
Jumanne 2 Februari 2016
[Mechi kuanza Saa 4 Dak 45 Usiku]
Arsenal v Southampton              
Leicester v Liverpool                  
Norwich v Tottenham                 
Sunderland v Man City               
West Ham v Aston Villa              
[Mechi kuanza Saa 5 Usiku]
Crystal Palace v Bournemouth               
Man United v Stoke          
West Brom v Swansea                
Jumatano 3 Februari 2016
[Mechi kuanza Saa 4 Dak 45 Usiku]
Everton v Newcastle         
Watford v Chelsea     

Hakuna maoni: