Fainali ya UCL baina ya City vs Bayern – Huenda ikamfanya Pep Guardiola Ajiuzulu
Ikitokea City na Bayern Munich wakakutana kwenye fainali ya tarehe 28 mwezi ujao, Guardiola atakuwa mpinzani wa waajiri wake wapya katika kugombea ubingwa mkubwa zaidi katika historia ya Manchester City.
sio tu atakuwa katikati ya ndoto za matajiri wa City kutwaa UCL bali pia kujipa wakati mgumu msimu ujao kwa kutoshiriki UCL, kutokana na haya kuna uwezekano akawa kwenye presha kubwa ya kujiuzulu kuifundisha Bayern Munich kabla ya mchezo wa fainali.
Guardiola ataingia kwenye mechi hiyo akijua kwamba ushindi utamaanisha kwamba hatoshiriki kwenye michuano hiyo msimu ujao, wakati akijua kipigo kwa Bayern kitamaanisha kwamba City watakuwemo msimu ujao kuutetea ubingwa wao.
Kwa hakika Guardiola atakuwa kwenye wakati mgumu na sijui kwa namna gani nyingine ataondoka kwenye mgongano huo, hata kama hakuna shaka anataka kuondoka Bayern akiacha legacy kubwa kwa kutwaa kombe hili.
Anaweza kuingia kwenye mchezo huo na kwa bahati mbaya mbinu zake zikazidiwa na kocha mwenzie na kupoteza bahati mbaya, kwa hakika maneno yatakuwa mengi.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni