Listi ya vilabu tajiri duniani, Madrid, Barca zaongoza, Man Utd yaongoza kwa kuingiza faida kubwa
Mapato makubwa ya fedha zinazotokana na mauzo ya haki za matangazo ya TV , mauzo jezi na mapato ya udhamini wa jezi, wadhamini na ushiriki wa Champions league umeendelea kuzipa uthamani mkubwa vilabu vya soka duniani.
UEFA imeongeza malipo katika Champions League kwa asilimia 50% kwa miaka 3 kuanzia msimu wa 2015-16. Fainali ya mwaka huu, itakayochezwa San Siro jijini Milan, Italy, baina ya vilabu vya Spain, Real Madrid vs Atletico, kila timu itapata kiasi cha $100 million.
Vilabu 20 ambavyo vinaongoza kwa uthamani vina thamani ya wastani wa $1.44 billion, ongezeko la 24% kuliko ilivyokuwa miaka 20 iliyopita. Malipo makubwa ya dili za TV, kama mkataba wa miaka wa miaka 3 wenye thamani ya $7.9 billion baina ya English Premier Keague na Sky Sports na BTSport ambao unaanza msimu wa 2016/17, na dili nyingine za udhamini wa jezi, mfano ukiwa mkataba wenye thamani ya $130m kwa mwaka baina ya Manchester United na Adidas.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni