La Liga: Miaka 23 ya kumbukumbu Mbaya Ya Siku Ya Mwisho Ya ligi Kwa Madrid – Wataandika Historia Mpya?
Real Madrid bado wana nafasi ya kushinda ubingwa wao wa 33 wa ligi siku tatu zijazo lakini wana kumbukumbu mbaya za kugombea ubingwa mpaka siku ya mwisho ya ligi.
Los Blancos’ ‘Dream Team’ iliyokuwa na wachezaji kama Fernando Hierro na Gheorghe Hagi walielekea Tenerife katika uwanja wa Estadio Heliodoro Rodriguez Lopez wakihitaji ushindi ili kushinda ubingwa wao 26 wa ligi.
Hierro na Hagi walianza kufunga kwa upande wa Madrid lakini mambo yakabadilika na balaa likahamia upande wa Los Blancos.
Barcelona wakaenda kushinda ubingwa baada ya kuwafunga Athletic Club 2-0 katika dimba la
Bernabeu baada ya Tenerife kurudi mchezoni na kuwafunga Real 3-2.
Barcelona wakaenda kushinda ubingwa baada ya kuwafunga Athletic Club 2-0 katika dimba la
Bernabeu baada ya Tenerife kurudi mchezoni na kuwafunga Real 3-2.
Kumbukumbu mbaya haishii hapo, historia ikajirudia na kuja kuwaandama tena Real Madrid msimu uliofuatia – walipocheza mechi ya mwisho tena na Tenerife.
Madrid wakafungwa 2-0 na Tenerife huku Barcelona wakishinda mechi ya mwisho na kubeba ubingwa wa pili mfululizo kwa tofauti ya pointi 1. Huu ulikuwa ubingwa wa 13 wa Barcelona.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni