LA LIGA: BARCA, REAL ZAKABANA KILELENI!
Mapema Jana Real Madrid walizoa ushindi mwishoni
walipoibwaga Valencia huko Santiago Bernabeu wakati Bao 2 za Luis Suarez
zikiisaidia Barcelona kuibwaga Espanyol katika Dabi ya Catalunya huko
Mjini Barcelona.
Huko Bernabeu, Cristiano Ronaldo aliipati Real Bao Dakika ya 27 alipounganisha kwa Kichwa Krosi ya Dani Carvajal lakini Kipindi cha Pili alikosa kufunga Bao la Pili wakati Penati yake ilipookolewa na Kipa Diego Alves.
Huko Bernabeu, Cristiano Ronaldo aliipati Real Bao Dakika ya 27 alipounganisha kwa Kichwa Krosi ya Dani Carvajal lakini Kipindi cha Pili alikosa kufunga Bao la Pili wakati Penati yake ilipookolewa na Kipa Diego Alves.
Dani Parejo akaisawazishia Valencia Dakika ya 82 kwa
Frikiki lakini Dakika 4 baadae Marcelo akafunga Bao la Pili na kuipa
Real ushindi wa 2-1.
Nao Barca wametwaa uongozi wa La Liga mbele ya Real baada kuichapa Espanyol 3-0 kwa Bao 2 za Luis Suarez na 1 la Ivan Rakitic.
Atletico Madrid wameichapa Las Palmas 5-0 na kujichimbia Nafasi ya 3 kwenye La Liga.
Atletico Madrid wameichapa Las Palmas 5-0 na kujichimbia Nafasi ya 3 kwenye La Liga.
Bao za Atletico zilifungwa na Kevin Gameiro, Bao 2, Saul, Thomas Parteyna Fernando Torres.
Tony Adams, Mchezaji wa zamani wa Arsenal, Jana alishuhudia Timu yake Granada ambayo yeye ndie Kocha wa muda ikiungana na Osasuna kuwa Timu ya Pili kushuka Daraja walipifungwa 2-1 na Real Sociedad.
Tony Adams, Mchezaji wa zamani wa Arsenal, Jana alishuhudia Timu yake Granada ambayo yeye ndie Kocha wa muda ikiungana na Osasuna kuwa Timu ya Pili kushuka Daraja walipifungwa 2-1 na Real Sociedad.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni