Totti Totti Totti jina linaloandikwa kila mahala mtandaoni.
Baada ya siku ya Jumapili mchezaji Fransesco Totti kucheza mchezo wake wa mwisho katika soka, watu mbalimbali wamekuwa wakimtumia salamu mchezaji huyo na kumuambia jinsi gani watamkumbuka.
Katika mtandao wa twitter kulikuwa na hashtag ya #Totti karibia kila ukurasa wa masuala ya soka duniani na hii ilionesha ni kwa jinsi gani Totti alikuwa akikubalika.
Mmoja kati ya watu ambao hawakusita kuonesha hisia zao mtandaoni ni mwanasoka Gervinho ambaye kupitia ukurasa wake wa Twitter aliandika “kati ya vitu ninajivunja ni kucheza na Totti,asante capitano mfalme wa Roma”
Lakini beki wa klabu ya Real Madrid Sergio Ramos amesema Totti kwa uwezo wake kila klabu duniani ingependa kuwa naye na akapost picha yake na kuandika Capitano.
Televisheni maarufu nchini Italia ya Itv imesema kupitia mtandao wa Twitter kwamba kuanzia sasa ligi kuu nchini Italia haitakuwa sawa kwani haiwezi kuwa sawa bila kuwepo kwa Fransesco Totti.
Klabu ya Inter Millan nayo imesema haiwezi kusahau jinsi Totti alibyokuwa akienda San Siro na watamkumbuka sana katika kipindi ambacho hayupo.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni