UEFA EUROPA LIGI-FAINALI MAN UNITED NA AJAX REFA NI YULE ALIEPONDWA NA MOURINHO!!
MGAO TIKETI KILA TIMU 9,500 TU!
Uteuzi huu huenda usimfurahishe Meneja wa Man United Jose Mourinho kwani aliwahi kumbatukia Refa huyo na kumwita ‘dhaifu’ na ‘asiejua kitu’ baada ya Refa huyo ‘kuidhulumu’ Chelsea Penati ya wazi Mwaka 2015 walipocheza na Dynamo Kiev.
Refa Skomina pia ashawahi kuichezesha Man United Mwaka 2012 Uwanjani Old Trafford walipofungwa 2-1 na Ajax kwenye Mechi ya EUROPA LIGI lakini wakasonga kwa Jumla ya Mabao 3-2.
TIKETI ZA FAINALI
Wakati huo huo, UEFA pia imetangaza mgao wa Tiketi za Fainali hii ambapo Manchester United will receive no more thanitapa si zaidi ya Tiketi 9,500 kwa Washabiki wake idadi ambayo Ajax pia watapewa.
Fainali hii itachezwa Uwanja wa Friends Arena Mjini Stockholm unaopakia Watu 50,000.
Idadi ya Tiketi zilizobaki zitauzwa Mtandaoni kwa Washabiki huko Sweden, Vyama vya Soka vya Nchi husika, Washirika wa Kibiashara wa UEFA, Watangazi wa TV/Radio wa Mechi hiyo na Kampuini maalum za kuhudumia Wateja.
UEFA EUROPA LIGI
FAINALI
24 Mei 2017: Friends Arena, Solna, Sweden
Ajax Amsterdam v Manchester United
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni