tecno

tecno

airtel

airtel

.

.

nido

nido

RADIO LISTEN NOW

12 Mei 2017

UEFA EUROPA LIGI: FAINALI NI MAN UNITED NA AJAX!!

Nusu Fainali – Mechi za Marudiano
**Kwenye Mabano Jumla ya Magoli kwa Mechi Mbili
Alhamisi Mei 11
Manchester United 1 Celta Vigo 1 [2-1]
Olympique Lyonnais 3 Ajax Amsterdam 1 [4-5]
++++++++++++++++++++++++
MANUNITED-FELLAINI-FAINALIManchester United na Ajax Amsterdam zimetinga Fainali ya UEFA EUROPA LIGI baada kupeta Mechi zao za Marudiano za Nusu Fainali.

Man United walitoka Sare 1-1 na Celta Vigo na wao kusonga kwa Jumla ya Bao 2-1 kwa vile walishinda 1-0 Wiki iliyopita huko Spain wakati Ajax wamefungwa 3-1 lakini wamesonga kwa Jumla ya Bao 5-4 baada ya kushinda Mechi ya Kwanza 4-1.
Man United walitangulia kufunga Dakika ya 17 kwa Bao la Kichwa la Marouane Fellaini alipounganisha Krosi ya Marcus Rashford.

Celta Vigo walisawazisha Dakika ya 86 kwa Bao la Kichwa la Fancundo Roncaglia.
Dakika chache baada ya Bao hilo la kusawazisha, Refa aliwatoa kwa Kadi Nyekundu Eric Bailly wa Man United na Roncaglia kwa kuvaana.

VIKOSI:
MAN UNITED: Romero; Valencia, Bailly, Blind, Darmian; Fellaini, Herrera, Pogba; Lingard [Rooney, 88’], Mkhitaryan [Carrick, 77], Rashford Smalling, 88]
Akiba: De Gea, Jones, Smalling, Carrick, Mata, Rooney, Martial

CELTA VIGO: Alvarez; Mallo, Cabral, Roncaglia, Jonny; Wass [Jozabed, 45], Radoja [Bongonda, 67], Hernandez; Aspas, Guidetti, Sisto [Beauvue, 79’]
Akiba: Villar, Fontas, Diaz, Bongonda, Beauvue, Jozabed, Gomez

REFA: Ovidiu Alin Hategan [Romania]
UEFA EUROPA LIGI
Tarehe Muhimu:
FAINALI
24 Mei 2017: Friends Arena, Solna, Sweden

Hakuna maoni: