Hizi anazofanya Pep Gurdiola sokoni sasa ni fujo
Baada ya dirisha la usajili tu kuanza Gurdiola akawapiga bao Real Madrid na Manchester United kwa kumnunua kiungo wa Monaco Bernardo Silva kwa dau la £43m.
Baada ya kumnunua Bernardo Silva siku kadhaa baadae ndani ya wiki moja Gurdiola kahamia kwa golikipa wa Benfica Ederson ambapo anatarajia kuwa golikipa ghali katika ulimwengu huu wa soka.
Gurdiola amepewa jina jipya la “Mr Cheque Book” jina ambalo amelipewa siku za hivi karibuni kutokana na pesa anazomwaga tu kwa kila mchezaji ambaye anamtaka.
Wakati suala la golikipa Ederson likikamilika tayari habari mpya kutoka familia za mwanasoka anayekipiga katika klabu ya Monaco Benjamin Mendy amekubali kujiunga na klabu ya Manchester City.
Picha za Mendy akiwa katika ndege binafsi siku ya Junapili inahisiwa alikuwa akienda Uingereza ili kukamilisha taratibu za mwisho za usajili wake kwenda Manchester City.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni