tecno

tecno

airtel

airtel

.

.

nido

nido

RADIO LISTEN NOW

28 Juni 2015

ARTURO VIDAL ASHAUZWA!

arturo-vidal1Huku kukiwa na habari kuwa Arsenal imeshailipa Juventus Dau la Pauni Milioni 21.3 kumnunua Kiungo wa Chile Arturo Vidal, Gazeti la kuaminika la huko Spain Marca limedai Staa huyo ameuzwa kwa Klabu kubwa Ulaya ambayo itatajwa baada ya Copa America kumalizika.
Hivi sasa Vidal, ambae Wiki iliyopita huko kwao Chile alifunguliwa mashitaka ya kuendesha Gari huku akiwa amelewa na kusababisha ajali, yuko huko huko Chile akiichezea Nchi yake inayoshiriki Copa America ambapo Jumanne Usiku itacheza Nusu Fainali na Peru.
Licha ya Marca kudai Klabu ambayo Juve imemuuza Vidal ni siri, habari zilizozagaa zinadai Mchezaji mwingine wa Chile anaechezea Arsenal, Alexis Sanchez, ndie aliemfanya Vidal aamue kwenda Arsenal.
Vidal ni mmoja wa Wafungaji Bora wa Copa America akiwa na Bao 3 na alianzia Soka lake la Kulipwa akiwa na Klabu ya Colo-Colo ya Chile Mwaka 2005 hadi 2007 alipohamia Bayer Leverkusen ambako alicheza Mechi 117 na kufunga Bao 15 kisha Mwaka 2011 kwenda Juventus alikocheza Mechi 124 na kufunga Bao 35.

Hakuna maoni: