tecno

tecno

airtel

airtel

.

.

nido

nido

RADIO LISTEN NOW

28 Juni 2015

EURO U-21: PORTUGAL YAIBONDA GERMANY 5-0, FAINALI KUIVAA SWEDEN!

EUROU21Portugal itakutana tena na Sweden katika Fainali ya Mashindano ya Nchi za Ulaya kwa Vijana chini ya Miaka 21, EURO U-21, huko Nchini Czech Republic baada zote Jana kushinda kwa kishindo Mechi zao za Nusu Fainali.
Portugal wametinga Fainali kwa kuibonda Germany 5-0 na Sweden wamewachapa jirani zao Denmark 4-1.
Portugal na Sweden walikuwa Kundi moja kwenye Mashindano haya na kutoka Sare 1-1.
Bao za Portugal, chini ya Kocha Rui Jorge, katika Mechi yao na Germany zilifungwa na Bernardo Silva, Ricardo, Ivan Cavaleiro katika Kipindi cha Kwanza na João Mário na Ricardo Horta kufunga Kipindi cha Pili.
Baada ya kuwa nyuma 5-0, Germany, walibaki Mtu 10 baada ya Leonardo Bittencourt kupewa Kadi Nyekundu.
Nao Sweden waliongoza 2-0 hadi Haftaimu kwa Bao za Penati ya John Guidetti na Simon Tibbling na Kipindi cha Pili kuanza kwa Denmark kupata Bao lao moja kupitia Uffe Bech lakini Sweden waliongeza 2 nyingine kupitia Robin Quaison na Oscar Hiljemark na kushinda 4-1.
Fainali ya U-21 itachezwa Jumanne Juni 30 na kuzikutanisha Swden na Portugal ambayo mara ya mwisho kucheza Fainali kama hii ni Mwaka 1994 
wakiongozwa na Chipukizi Luís Figo na Rui Costa ambao waliibuka kuwa Masupastaa wa Dunia.
MAKUNDI
KUNDI A
**Kila Timu imecheza Mechi 3
1 Denmark Pointi 6
2 Germany 5 
3 Czech Rep 4
4 Serbia 1
KUNDI B
**Kila Timu imecheza Mechi 3
1 Portugal Pointi 5
2 Sweden 4
3 Italy 4
4 England 3
****Timu 2 za juu za kila Kundi zitasonga Robo Fainali
RATIBA/MATOKEO:
**Mechi zote Saa 3 Dakika 45 Usiku
Jumapili Juni 21
Sweden 0 England 1
Italy 0 Portugal 0
Jumanne Juni 23
Czech Republic 1 Germany 1
Denmark 2 Serbia 0
Jumatano Juni 24
England 1 Italy 3
Portugal 1 Sweden 1
NUSU FAINALI
Jumamosi Juni 27
Demark 1 Sweden 4
Germany 5 Portugal 0
FAINALI
Jumanne Juni 30
Portugal v Sweden

Hakuna maoni: