tecno

tecno

airtel

airtel

.

.

nido

nido

RADIO LISTEN NOW

22 Juni 2015

JEURI YA REAL, KIBURI CHA MAN UNITED-UNAMTAKA DE GEA, TUPE RAMOS!

SERGIO-RAMOSNi wazi imeibuka vita ya chini kwa chini kati ya Vilabu vikubwa Barani Ulaya, Real Madrid na Manchester United, David-de-Gea-shangiliasakata ambalo lilianza kwa Real kumtaka Kipa wa Man United David de Gea.
Akiwa amebakisha Mwaka mmoja kwenye Mkataba wake na Man United, David de Gea alipewa Mkataba mpya ulioboreshwa lakini akawa anasita kuusaini na kuibuka ripoti kuwa anataka kurudi kwao Spain kuidakia Real Madrid.
Wakati hilo likonekana halikwepeki Man United nao wakajibu mapigo kwa kuripotiwa wakitaka dili yeyote ya David de Gea ihusishe na wao kupewa Mchezaji na sasa Beki Sergio Ramos ndie ameibuka mlengwa.
Lakini habari za ndani ya Real zinadai Ramos hawezi kwenda kokote kwa vile Mkataba wake wa sasa unaoisha 2017 una kipengele cha Real kulipwa Euro Milioni 200 ikiwa atahama kabla Mkataba kwisha.
Vile vile, Real wanaamini wao watampata De Gea na Ramos hataenda kokote kwa vile nia yake si kuhama bali ni kuboreshewa Mkataba wakati De Gea anataka kuhama ili arudi kwao.
Hata hivyo, Real wanasemekana kukiri kuwa mambo ni magumu kwani Man United hawataki mazungumzo yeyote kwa wakati huu.

Hakuna maoni: