tecno

tecno

airtel

airtel

.

.

nido

nido

RADIO LISTEN NOW

24 Juni 2015

OFFICIAL: LIVERPOOL YAIZIDI KETE MAN UNITED KWA KUMSAJILI STRAIKA HUYU….

LONDON, ENGLAND - MARCH 29:  Firmino of Brazil celebrates after scoring the opening goal during the international friendly match between Brazil and Chile at the Emirates Stadium on March 29, 2015 in London, England.  (Photo by Paul Gilham/Getty Images)
LONDON, ENGLAND – MARCH 29: Firmino of Brazil celebrates after scoring the opening goal during the international friendly match between Brazil and Chile at the Emirates Stadium on March 29, 2015 in London, England. (Photo by Paul Gilham/Getty Images)
Liverpool imethibitisha rasmi kumsajili mshambuliaji wa Brazil, Roberto Firmino kutoka klabu ya Hoffenheim kwa dau la paundi milioni 29.
Firmino mwenye miaka 23 amesaini mkataba wa miaka mitano ambao atakuwa akilipwa mshahara wa paundi laki moja kwa wiki na anaungana na Wabrazil wenzake Anfield, Philippe Coutinho na Lucas Leiva
Hata hivyo, Firmino haendi kuchukua vipimo vya afya mpaka Brazil itakapotoka kwenye michuano ya Copa America inayoendelea nchini Chile.
Mshambuliaji huyo anakuwa mchezaji wa pili kusajiliwa na Majogoo kwa dau kubwa zaidi kihistoria kwani Andy Carroll, alisajiliwa kwa paundi milioni 35 mwezi Januari 2011 
Mkurugenzi mkuu wa Liverpool, Ian Ayre alisafiri mpaka Chile usiku wa kuamkia leo na kukamilisha usajili wa Firmino ambaye alikuwa anawindwa pia na Manchester United.
Hii ndio Tweet ya Liverpoool asubuhi hii:

Hakuna maoni: