tecno

tecno

airtel

airtel

.

.

nido

nido

RADIO LISTEN NOW

24 Julai 2015

WENGER AICHOKONOA MAN UNITED-'IMETUPA UTAMADUNI WAKE KUSAKA UTUKUFU!'

reu 189524MENEJA wa Arsenal Arsene Wenger amehoji msimamo wa Manchester United katika Uhamisho wa Wachezaji kwa kudai 'imetoa kafara Utamaduni wake kwa kusaka Utukufu.'
Katika kipindi hiki cha Dirisha la Uhamisho, Man United imetumia karibu Milioni 80 kuwanunua Wachezaji Wanne ambao ni Memphis Depay, Matteo Darmian, Bastian Schweinsteiger na Morgan Schneiderlin wakati Arsenal imenunua Mchezaji mmoja tu, tena Mkongwe, Kipa Petr Cech, kutoka Chelsea kwa Pauni Milioni 10.
Wenger, ambae husifika kwa ubahili katika kununua Wachezaji, anahisi kutanua Misuli ya Fedha kwa Man United kunaathiri kukuza vipaji vya Wachezaji Chipukizi na pia anaamini hima ya Meneja wao Louis van Gaal kununua Wachezaji ni dalili Klabu hiyo imepoteza uvumulivu.
Wenger ameeleza: "Sisi tutaendeleza kuchanganya uwezo wetu Kifedha na imani yetu katika Falsafa na Sera ya kuwapa nafasi Wachezaji Chipukizi na kukuza Wachezaji toka ndani ya Klabu kama Utamaduni wetu ulivyo. Kama baada ya hapo tutashindania kununua Wachezaji sawa lakini huo hautakuwa msingi wa Sera yetu."
Wenger amefafanua: "Klabu karibu zote zilizokuwa na mafanikio zilifanya hivyo. Zichukulie Barcelona na Man United, ambao walikuwa na kizazi kilichokuzwa toka ndani ya Klabu. Hilo ndio utamaduni wetu na ni muhimu kubakiza hivyo. Hilo liliwapa Man United mafanikio na kutengeneza Fedha nyingi lakini Leo hawana uvumilivu kuendeleza hilo hilo. Wana uwezo Kifedha kufuata Sera nyingine. Na sasa hawana kizazi cha Wachezaji kama Paul Scholes, Ryan Giggs na David Beckham ndani ya Klabu yao."

Hakuna maoni: