tecno

tecno

airtel

airtel

.

.

nido

nido

RADIO LISTEN NOW

1 Septemba 2015

DIMARIA ATAJA KILICHOMUONDOA MANCHESTER UNITED

Angel Di Maria wakati akikipiga Manchester United kabla ya kuhamia PSG ya Ufaransa
Angel Di Maria wakati akikipiga Manchester United kabla ya kuhamia PSG ya Ufaransa
Baada ya kucheza kwa msimu mmoja tu katika klabu ya Manchester United, winga Angel Di Maria amefunguka na kumtaja kocha Louis Van Gaal kuwa ndiye sababu ya yeye kuondoka.
Akizungumza kupitia ESPN winga huyo anayekipiga PSG hivi sasa anasema, “Van Gaal ana filosofia yake, na ndio ilikua kikwazo kwangu. Nilifurahia maisha Old Trafford lakini mambo yalibadilika baada tu ya kuumia ankle yangu na kocha kunibadilisha nafasi ya kucheza uwanjani”.
Di maria anasema alishindwa kuitumikia falsafa ya Louis Van Gaal na alipompigia simu Blanc (kocha wa PsG) alimuhakikishia kumchezesha alivyokuwa akicheza Real Madrid.
Angel Di Maria aliweka rekodi ya uhamisho kwa vilabu soka nchini England baada ya kusajiliwa kwa ada ya uhamisho wa pauni milioni 60 akitokea Real Madrid

Hakuna maoni: